Loading...

SPONSOR THINGS: HERE is what to do after you hit 40 years and NO SPONSOR WANTS YOU!

 SPONSOR THINGS: HERE is what to do after you hit 40 years and NO SPONSOR WANTS YOU!
By Hon Jim Bonnie
When you’re still young, beautiful and energetic, you shun young men as you go for sponsors from whom you get money to buy Brazilian hair, chemicals to bleach your skin and makeup to make you look like Angelina Jolie yet you look like Kibaki.
You hit 30, the sponsors start running away from you to hunt for younger ladies for you’ve hit your expiry date in the shelf of sponsorship.
The number of abortions you’ve carried out outnumber the number of times you’ve had sex and your breasts look like you’ve breastfed eleven kids.
You’re also facing financial crunch as there are no more sponsors in the market to milk. Uko down financially. All your undies don’t fit for the fake booty maintained by sponsor’s cash has shrunk.
Too bad you never used money from them to start a business of your own or advance your career.
All you were doing is shop for expensive dresses and expensive alcohol to show the world that you’re on top game. You even thought ladies sweating their ass off to feed their families are fools.
The reality starts dawning on you that you wasted away in leisure. Neither the sponsors want you because you’re a spent cartridge nor the young men for you look like the devil out of the woods.
Of course you’ve no friends because you were rolling big and you saw no need of being in the company of foolish poor people. So, your only option is to get comfort in marriage.
You can’t ask for it on social media because we know you and how you were showing us photos of your buttocks after enjoying sex with octogenarian sponsors.
So you erect billboards on the streets with the hope that you’ll land a man who doesn’t know you.
You’re also very clever. You don’t include your tattered image. All you need is a man. You don’t care whether he pulls a cart or hustles in industrial area.
When you fail to get one, you start calling men Dogs. Idiot.
271

Kajala Akanusha Kutoka Kimapenzi na Msami



Kajala na Msami Katika Pozi
Msanii wa filamu Kajala Masanja amekanusha tetesi za kwenye mitandao ya kijamii kuwa anatoka kimapenzi na mkali wa wimbo ‘Mabawa’, Msami.
kajala

Mwingizaji huyo ambaye hivi karibuni ilisambaa video inayomuonyesha akidendeka na rapa Quick Rocka, ameiambia Clouds Fm kuwa Msami ni mshkaji wake wa karibu sana na sio mpenzi wake.

“Unajua kuna watu wanaweza wakawa labda ni washikaji au wana vitu vingi pembeni lakini watu wengine hawajui, mi na Msami ni washkaji sana,” alisema Kajala.

Aliongeza, “Halafu sio kila siku watu watakuwa wanatuona barabarani au tunapostiana picha kwenye Instagram, lakini mimi na yeye tunaongea vitu vingi, kwa hiyo imekuwa rahisi mimi kuacha usingizi wangu kuja kwa Msami, sina uhusiano naye na vitu vingine mtavijua baadaye.”

Wawili hayo wamekuwa wakioneka wakiwa pamoja mara nyingi hali ambayo imeibua hisia huenda wakawa wanatoka kimapenzi.

Ndoa ya Mwanamuziki Steve R n'B Chali..Mwenye Adai Hana Bahati...



Steve Rn'B akiwa na aliyekuwa mke wake.
Pia Steve amesema alifanikiwa kupata mtoto mmoja katika ndoa yake na kusema ndoa ni kati ya watu wawili hivyo makubaliano ya kuachana yalikuja baina yao na pia itakapofikia wakati wa kurudiana wataamua wao.

Steve amesema anatarajia kuachia ngoma yake mpya ambayo amemshirikisha Bell Nass na kusema ndani ya ngoma hiyo watu watarajie kupata ladha na ubunifu kama ilivyo kawaida yake akidai kuwa huwa hakosei anapoamua kuachia ngoma.

Rama D Afunguka Kuhusu Yeye na Lady Jay Dee

Mwanamuziki wa R&B nchini Tanzania Rama D, amekanusha vikali habari zilizotapakaa mtandaoni kwamba kwa sasa anatoka kimapenzi na mwanadada Lady Jay Dee, amesema wanaheshimiana sana na haiwezi kutokea kitu kama hicho daima .

Hata hvyo Rama D ameendelea kusema kwamba yeye anamfaham mpaka mpenzi wa mwanadada Lady Jay Dee na kusema hata siku ya show ya ‘Naamka Tena Concert’ alipanda jukwaani kuonesha jinsi anavyomkubali mwana dada huyo.

Rama D anasema anawashangaa sana watu wanaoenda kufanya video zao nje na kusema kwamba haoni sababu ya kufanya video hizo nje kwani hapa nyumbani kuna mazingira ya kutosha kufanya video nzuri zitakazoitangaza nchi.

Naumia Sana Pale Mwanangu Sasha Anapouliza Kuhusu Baba yake – Faiza Ally

Aliyekuwa mke wa Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye pia ni msanii wa filamu, Faiza Ally amefunguka na kueleza kitu ambacho kinamnyima furaha maishani mwake.
Faiza na mtoto wake Sasha

Muigizaji huyo ambaye aliachana na mume wake ambaye ni mbunge Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, amekuwa akilalamika mara kadhaa kuhusu mume wake huyo ambaye alifanikiwa kuzaa naye mtoto mmoja aitwae Sasha.

“Jambo linalonipa huzuni mara kwa mara ni pale mwanangu Sasha anaponiuliza habari za baba yake, huwa naumia mno. Ila tukio la furaha ambalo siwezi kulisahau ni pale nilipopata uchungu wa dakika kadhaa lakini nilikuja kupata furaha ya maisha yangu yote siku nilipo jifungua, Sasha,” Faiza aliliambia gazeti la Mtanzania.

Hata hivyo, Faiza aliwahi kukaririwa akisema kuwa yupo tayari kuzaa mtoto mwingine na Sugu lakini sio kurudiana naye.

Baraka da Prince Afunguka Kuhusu Yeye na Linah Baada ya Picha ya Utata Kuzagaa Mtandaoni

Msanii Baraka da Prince amekanusha vikali kumshika msanii wa kike wa bongo fleva sehemu za kifuani, na kusema aliyepiga picha hiyo aliikuza.

Akiongea kwenye eNews ya East Africa TV, Baraka amesema hajwahi kufanya kitendo kama hicho kwani walikuwa sehemu yenye watu wengi, na pia hajawahi kuwaza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Linah.

“Siwezi kufanya kitu kama hicho kwa sababu pale pana watu wengi, ile picha ilikuwa ya kawaida, yule aliyeipiga na kuipost amekuwa kama kaikuza, sijawahi kufikiria hata kutoka naye”, alisema Baraka.

Pia Baraka amesema siku ya tukio ambayo ilikuwa ni siku ya kuadhimisha miaka 10 ya muziki wa Christian Bella, aliondoka mapema na hakufanya tukio lolote baya.

“Nimetoka kuperfom nikaondoka zangu, sikukaa hata nusu saa, nimemaliza nikaondoka, wasiwe wanaamini mambo ya hivyo”, alisema Baraka.

Ni halali wapenzi wa jinsia moja kuchunguzwa kimatibabu Kenya

 
Mahakama moja nchini Kenya imetupilia mbali kesi ya kikatiba iliyokuwa ikipinga uhalali wa uchunguzi wa tupu ya nyuma kama idhibati ya ngono ya wapenzi wa jinsia moja.
Mahakama kuu ya Mombasa imesema kuna sheria fulani nchini Kenya inayohalalisha uchunguzi kama huo kwa sababu za kutafuta ushahidi. Kwenye uamuzi wake, hakimu Mathew Emukule alisema kulikuwa na ruhusa fulani kwenye sheria za Kenya kuchunguza maumbile ya binadamu kwa lengo la kutafuta ushahidi wa hatia kama unajisi au kuficha madawa ya kulevya.
Aidha alitupilia mbali wazo kuwa uchunguzi kama huo unabagua kijinsia, akisema kuwa tupu ya nyuma si ya kijinsia bali ni ya utumbo. Aidha alisema uchuguzi kama huo ulikubalika kwani walalamishi walikubali kufanyiwa.
Hatua hiyo inajiri baada ya wanaume wawili kuwasilisha ombi la kikatiba wakisema walifanyishwa uchunguzi wa kimaumbile sawa na virusi vya ukimwi na hepatitis, walipokamatwa kwa shutma za mapenzi ya jinsia moja mnamo Februari mwaka jana.
Mapenzi ya jinsia moja ni hatia nchini Kenya, na adhabu yake ni kifungo gerezani kwa muda usiozidi miaka kumi na nne.

Watuhumiwa wa Ubakaji na Waliosambaza Picha za Uchi za Msichana Morogoro Waendelea Kusota Rumande

Waendesha mashtaka wa serikali Morogoro wamepewa miezi miwili kuwasilisha cheti kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ili kuachia ama kuendelea kushikilia dhamana ya washtakiwa wanne wa kesi ya usambazaji wa picha chafu za ngono.

Washtakiwa hao ni wale waliopiga picha chafu za ngono dhidi ya mwanamke mmoja mkazi wa Kijiji cha Dakawa, Mvomero.

Mbele ya waendesha mashtaka wa serikali Gloria Rwakibalila, Edgar Bantulaki na Calistus Kapinga ilidaiwa mahakamani hapo na Ivan Msacky, Hakimu wa Mahakama hiyo kuwa, suala la dhamana chini ya Katiba ni haki ya kila mshtakiwa lakini akaonesha kushangazwa na upande wa mashtaka kutoeleza kwa uwazi sababu za kuendelea kuizuia dhamana hiyo.

Hakimu Msacky amewataka waendesha mashtaka hao kuhakikisha wanawasilisha mahakamani cheti kinachozuia dhamana kwa washtakiwa hao na sababu zake ili kesi hiyo iweze kuanza kusikilizwa.

Kesi hiyo ya jinai namba 54 ya mwaka 2016 inawakabili washtakiwa sita ambao ni Idd Adam Mabela, Zuberi Thabit, Rajab Salehe, Ramadhani Ally, Muksin Ng’ahy na John Peter ambao wanakabiliwa na shtaka la kusambaza picha chafu za ngono za msichana mwenye umri wa miaka 21 wilayani Mvomero mkoani humo. Washtakiwa wanaotaka dhamana ni mshtakiwa namba tatu hadi sita.

Hata hivyo, Hakimu Msacky jana aliahirisha kesi hiyo hadi tarehe 29 Juni mwaka huu ambapo kesi hiyo itaendelea kujadili suala la dhamana kwa washtakiwa hao.

Katika kesi hiyo iliyosikilizwa kwa mara ya kwanza tarehe 18 Mei mshtakiwa namba 1 na 2 wanatuhumiwa kumbaka na kumuingilia kinyume na maumbile msichana huyo Aprili 27, saa 1 usiku katika nyumba ya kulala wageni ya TITII iliyopo katika Tarafa ya Dakawa, Mvomero.

Katika kesi ya kwanza ya kubaka na kulawiti inayowakabili washtakiwa Mabela na Thabiti, wakazi wa jijini Mbeya ilishindwa kusikilizwa jana  kutokana na wakili wa washtakiwa Mohamed Mkali kutokuwepo mahakamani.

Mume Kamtegesha Mke Kwa Njemba ili Avute Hela ya Ugoni..Kilichotokea Hata Kaa Asahau

Hii muvi ilianza kuna jamaa alikuwa anafkuzia mke wa mtu bila kuchoka.
Mke akamwambia mume.wakashauriana waweke mtego matata wa kufumania ili mgoni abananishwe atoe pesa maana anazo!
Siku ikawadia mke akakubaliana na jamaa wakutane gesti kama kawaida wako ndani washavua kila kitu mara mara mwenye mke akavamia na jamaa yake ili wamtaiti mgoni!kumbe mgoni mjanja bana akawatolea bastola akawaamuru wafunge mlango afu akawaweka chini ya ulinzi na kuwafunga kamba alafu akaendelea kula mzigo mbele yao hadi akamaliza afu akawafungia wote humo ndani akasepa ..Jamaa akajikuta kakosa ela na mkewe katafunwa mbele yake.....

Exclusive: Wastara Juma Anasa Ujauzito.....

Exclusive! Habari mpya ya motomoto ni kwamba, staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma amenasa ujauzito, Risasi Jumamosi linakuwa la kwanza kukupa mchapo huu!
Ujauzito huo ni wa aliyekuwa mumewe, Sadifa Juma, mbunge wa Jimbo la Donge, Visiwani Zanzibar ambapo kitendo cha mimba hiyo kuwa ya mbunge, kimemsumbua Wastara hadi kuamua kuondoka ili akapate muda mzuri wa kutafakari nchini Msumbiji.

Taarifa kutoka kwa vyanzo, zinaeleza kuwa Wastara alipoondoka nchini, aliwaaga baadhi ya mastaa wenzake kuwa anakwenda kufuata biashara zake za nguo nchini humo lakini Risasi Jumamosi lilichimba na kupata ubuyu ulionyooka kuwa aliondoka nchini kwa ajili ya kwenda kutafakari ujauzito huo.

NDUGU AVUJISHA UBUYU KAMILI
Ndugu wa karibu na Wastara ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazeti, amefunguka kuwa baada ya Wastara kuachika, aligundua ni mjamzito hivyo alichanganyikiwa na kuamua kwenda Msumbiji kwa ajili ya kutafakari zaidi ujauzito huo.
“Hakuwa na jinsi kwani akiangalia alishatoka kwa mwanaume, angewezaje kumwambia kuwa ana ujauzito wake? Akaamua kukimbilia huko kwa ajili ya kujipanga ingawa anavyoonekana anatamani amzalie mbunge huyo,” alisema ndugu huyo.

NDUGU AZIDI KUTIRIRIKA
Ndugu huyo alizidi kushusha ‘vesi’ kuwa mimba ya Wastara inasadikiwa kuwa na miezi miwili au mitatu kwani tangu aachane na mumewe huyo, alikuwa akiumwaumwa na wakati mwingine alikuwa akitapika hovyo ambapo mwanzo alificha lakini yalipomfika shingoni alifunguka.
“Alitufichaficha lakini baadaye akawa hana jinsi, akaona atueleze na sisi tumemshauri tu aende akapumzike na ajiandae kutuletea kiumbe kipya,” alisema ndugu huyo.
Baada ya habari hiyo kutua Risasi Jumamosi,  Wastara alitafutwa kwa njia ya simu ya mkononi, akafunguka:

“Dah! Sijui niseme nini, kiukweli watu wanaongea sana, nimeondoka nchini kwa shughuli zangu binafsi lakini maneno ni mengi, wewe si wa kwanza kunipigia simu. Sikutaka kuongea kabisa juu ya masuala yangu ya ndoa iliyopita wala maisha yangu kwa jumla.”

Risasi Jumamosi: Kwa nini unaongea hivyo wewe funguka swali nililokuuliza, una ujauzito au la?
Wastara: Ndiyo, kwani cha ajabu ni nini? Yule niliyekuwa nalala naye si shangazi yangu, kila mtu anajua niliolewa na aliyenioa (Sadifa) wala si mjomba wangu.

TUJIKUMBUSHE
Wastara aliachika Aprili, mwaka huu baada ya kufunga ndoa na Mbunge wa Jimbo la Donge, Sadifa Juma ambapo ndoa yao ilidumu kwa muda kwa miezi mitatu tu na kuvunjika.

GPL

Nuh Mziwanda Amuumbua Upya Shilole

Msanii anayefanya poa kwenye Bongo Fleva, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ amemuumbua upya aliyekuwa mwandani wake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kwa kuanika A-Z ya namna alivyokuwa anamnyanyasa kwenye uhusiano wao wa kimapenzi kiasi cha kuamua kuachana naye. Wikenda limeinyaka.

Akizungumza na Wikienda mara baada ya kuachia video ya wimbo wake mpya wa Jike Shupa huku ndani yake akigusia kiduchu figisufigisu alizokutana nazo kwenye uhusiano huo akimtumia mrembo anayefanana na Shilole ‘Shilole bandia’.

Nuh aliliambia gazeti hili kuwa alishindwa kustahimili kuacha matukio ya uhusiano wake yapite hivihivi bila kuyagusia kidogo kwenye wimbo wake huo kwa sababu alihisi watu hawamuelewi kile alichokuwa anakisema juu ya Shilole.

“Nimeamua kufanya hivi ili Watanzania waone jinsi Shilole alivyokuwa ananifanyia kupitia mtiririko wa matukio kwenye kichupa changu. Kiukweli inaumiza sana lakini hivyo ndivyo roho yake ilivyo, sijali ataumbuka kwa kiasi gani lakini hizo ni hisia zangu ambazo nimeamua kuziweka upya,” alisema Nuh huku akiongeza kuwa kwa sasa yuko kwenye uhusiano na mwanadada aitwaye Nawal.

Hata hivyo, baada ya gazeti hili kuchonga na Nuh lilimtafuta Shilole ambaye alipoulizwa juu ya sakata hilo alidai kuwa hataki kumzungumzia Nuh wala kusikia habari zake maana hata video yenyewe hawezi kuiangalia.

“Sitaki kusungumzia habari za mtu mwingine, no coment, labda kama kuna ishu nyingine unaweza
kuniambia,” alisema Shilole. Shilole na Nuh waliachana miezi kadhaa iliyopita ambapo mrembo huyo alidai alikuwa akimlea jamaa huyo hivyo Nuh naye ameamua kueleza ukweli namna ambavyo Shilole aligeuka mwanamasumbwi ndani ya nyumba.

Wanandoa Waliodumu Muda Mrefu Kuanza Kupewa Tuzo Tanzania


Imezoeleka kwamba ndoa za kikatoliki zikifungwa zimefungwa lakini pamoja na sharti hilo idadi ya ndoa zinazovunjika inaendelea kuongezeka ambapo sasa kanisa katoliki limekuja na hii ya kuanzisha tuzo maalumu kwa Wanandoa wakongwe zaidi kwa mwaka huu katika kanisa hilo.
BBC SWAHILI wameripoti kwamba Kanisa Katoliki jimbo kuu la Dar es salaam limeandaa kliniki ya ndoa ili kuweza kuwapa fursa Wanandoa kuimarisha ndoa zao kiimani, Padre Novatus Mbaula ambaye ni mkurugenzi wa ndoa na familia anaeleza lengo la kliniki hii ni kuwapa nafasi wanandoa kupata neno la Mungu na kuweza kuongea juu changamoto zao mbalimbali kuongea kuhusu maisha yao ya ndoa.
Ni nafasi ambayo wanandoa ambao wana uzoefu mkubwa katika ndoa wanaweza kuwafaidisha wanandoa wachanga na miongoni mwa watu waliohudhuria kliniki hii ni wanandoa wenye ndoa yenye miaka 61, Brigedia Jenerali mstaafu Francis Mbena mwenye umri wa miaka 86 alifunga ndoa akiwa na miaka 25 mwaka 1965 June,anasema wao zamani walikua wanafuata mtu na familia gani na ina vigezo gani.
Walikua wanaangalia tabia kama msichana hana tabia nzuri huoi huko, kama familia ina watu walevi bali unatafuta familia yenye watoto wenye tabia nzuri ili na wewe uweze kupata watoto wenye tabia nzuri.
S

Baada ya FA Kupata Jiko… AY Naye Mbioni Kufunga Ndoa

KUFUATIA staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’ kufunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi, Helga wiki iliyopita, swahiba wake mkubwa, Ambwene Yessaya ‘AY’ amefunguka kuwa naye yuko njiani. Akizungumza na mtandao huu, AY anayebamba na Ngoma ya Zigo alisema kuwa ni jambo jema kwa rafiki na ndugu yake wa karibu (MwanaFA) kufunga ndoa hivyo imempa hamasa.

“Nimefurahi sana kwa swahiba wangu kufunga ndoa. Naamini FA amefungua ukurasa mpya katika maisha yake ya kuwa na mwenzake. Nami nipo njiani kumfuata Mungu akipenda,” alisema AY bila kumuweka wazi mwandani wake anayetarajia kufunga naye ndoa.

Umuhimu wa Kuhonga Katika Mapenzi...


1. KUHONGA HUBORESHA MAPENZI:

Fahamu kuwa unapomhonga mpenzi wako unamfanya ajihisi kama ni wapekee kwako, atajiona kama ni mmoja wapo kati ya watu wenye thamani kwako na huamini kama kweli upo karibu yake na unamjali.

Hali hii humfanya yeye kushindwa kutolipa mazuri kwako.
Wengi kabla ya kuomba papuchi hutanguliza hongo kwanza, si lazima iwe pesa hata hongo ya sifa za uongo na ukweli.

Kwa kuhonga kwako inamlazimu na yeye kulipa fadhila kwa kuonesha upendo wa dhati na utamfanya azidishe mapenzi kwako.

2. KUHONGA KUNAJENGA SANA KUMBUKUMBU KATIKA MAPENZI:
Fahamu kuwa unapomhonga mpenzi wako inakusaidia wewe kujijenga katika mawazo yake na endapo kama itatokea mkaachana nae basi pindi mpenzi wako atakapokuwa anaziona zawadi zako zitamfanya akukumbuke kwa mengi na atahisi kama kuachana na wewe kwake kuna tofauti na atajihisi kupoteza vingi toka kwako na kamwe kumbukumbu yako kwake haitofutika kila anapoona vitu ulivyomhonga.

Jitahidi sana unapohonga usihonge pesa tu, honga vitu vya kudumu maana huwa asset yako ya baadaye, pindi unapotokea mkwaruzano baina yenu.

Pesa huwa ni hongo inayovutia kwa muda mfupi na husaidia kupata kile unachokitaka kwa muda mfupi, ila jua atazitumia zitaisha utakuwa hujajenga misingi imara ya mapenzi.

Simaanishi kuwa usimpe mpenzi wako hela, hapana ila inabidi ufahamu kuwa pesa hutumika katika kukidhi mahitaji na sio katika kuboresha mapenzi.

Diamond Amuandalia Mwanaye Tiffah Birthday ya Kukata na Shoka itakayofanyika Mlimani City

Mwanamuziki Diamond amethibitisha habari kuwa amemuandalia mwanaye Tiffeh Birthday kubwa ya kukata na shoka, itakayofanyika mlimani City. 

Tiffah mwenye umri wa miezi 10, kwa sasa ana followers zaidi ya 623,049 Instagram, na inadaiwa kuwa ndiye superstar mdogo zaidi kwa Africa.

“Happy 10th Months my little Angel… can’t wait for your first year’s Birthday!!!!! Pale mlimani City patakuwa kama Disney Land!!!! @princess_tiffah,” ameandika Diamond kwenye Instagram.

Naye mama yake alimpongeza kwa kuandika: Yesterday you were mummy’s tiny baby and today you are mummy’s big girl. Happy 10 my beautiful princess the apple of my eye, the air I breathe. Plse don’t grow so fast, mummy will miss you being her baby.”

Staa wa Kenya, Huddah ni miongoni mwa mastaa walio na hamu kubwa ya kuwepo kwenye birthday hiyo.

“Our baby @princess_tiffah Turning ONE soon…. The ROYAL DUTCHESS of TZEE . Hii Sio party ya kikosa Jamani . There will be a BIG SURPRISE that day! Asiye na wake aeleke jiwe….Mimi I’ll be there na mawe zangu khaa! Mama Tiffa @zarithebosslady give us LOCATION Basi …. We need to book tickets EARLY,” aliandika.

The Ugly Truth: Wanaume Wote ni Malaya na Wasaliti - Dr. Mwaka

Mwanamke anaweza kuishi katika ndoa au mahusiano bila kucheat kwa asilimia 99 na wanaume wanaweza kuishi bila kucheat kwa asilimia 1 kwa sababu ni nature ya mwanaume kuwa hivyo.Kwahiyo ukiona mumeo au mpenzi wako hujamkamata inabidi umuheshimu saaana kwasababu anafanya kwa umakini na usiri wa hali ya juu ili asiumize hisia zako.wanaume wasiochet ni wale wagonjwa na makasisi wacha Mungu tu. Wengine wooote tupa kule.

Huu ndio ukweli mchungu kuhusu wanaume, Na ukweli unabaki palepale kuwa asilimia 99 ya wanaume wanatoka nje ya ndoa au mahusiano yao tena bila kuwa sababu ya msingi they just do haimaanishi kwa kufanya hivyo hawawapendi wake zao bali ni maumbile yao ndio yanawatuma hivyo. Kwahiyo kama umeolewa au una mpenzi ukimakamata na mwanamke mwingine usimhukumu kwa KUCHEAT bali mhukumu kwa KUCHEAT KIPUMBAVU mpaka akakamatwa wakati wenzake wanacheat na hawakamtwi.

najua kuna mikunguru minafiki itakuja hapa na kubisha ila ukweli ndio huo - By Dr JJ MWAKA

Hamisa Mobeto Amlipua Lulu Michael Kisa Kigogo Penzi la Kigogo

Mwanamitindo ambaye pia ni video queen maarufu Bongo, Hamisa Hassan Mobeto, amemlipua laivu staa wa filamu za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kisa kikidaiwa ni lile saga la kugombea penzi la kigogo (jina tunalo) ambapo kwa sasa hali ni tete baina ya wawili hao.

Hivi karibuni kuliibuka vita kali ya matusi mitandaoni kati ya kundi la mashabiki wa Hamisa linalojiita Team Hamisa na lile la Team Lulu ambapo kila kundi lilitaka kuibuka mshindi huku mada kuu ikiwa ni penzi la jamaa huyo.
Wakati hali ikiwa hivyo, ilibidi wawili hao nao kuvunja ukimya na kuanza kujibizana maneno ya nguoni ambayo yalizua taharuki upya kwa kila upande.

Baada ya kushuhudia malumbano hayo huku kukiwa na maelezo kuwa wawili hao wanachonganishwa, Wikienda lilimtafuta rafiki wa karibu wa Hamisa ili kuanika kiunaga ubaga hasira alizokuwa nazo Hamisa ndipo aliamua kufunguka kwa kumpa makavu Lulu. Mtu huyo alisema kuwa maneno aliyoyatumia Hamisa yalitokana na hasira na hayaandikiki gazetini huku akifafanua kuwa yeye ana mtoto lakini Lulu hana uchungu kwa kuwa bado hajazaa.

Baada ya kujazwa data hizo, Wikienda lilianza kwa kumtafuta Hamisa ili kupata ufafanuzi juu ya sakata hilo ambapo alisema kuwa utaratibu aliojipangia kwenye maisha yake ya siku hizi ni kutotoa taarifa zake kwa waandishi wa habari hivyo asingependa ‘ku-coment’ lolote juu ya hilo japokuwa kila suala lipo wazi.

“Kusema kweli maisha ya sasa kuna muda unaweza kujikuta ukiingizwa kwenye ugomvi ambao hukutarajia na hivyo kwa kuzingatia hilo nisingependa kuongelea tena habari hii maana utaratibu wangu ni kutotoa taarifa wala mambo yangu kuyaweka wazi kwenye magazeti ila kilichoonekana ndicho hicho kwa sasa sina coment yoyote,” alisema Hamisa.

Kwa upande wake Lulu alijibu mapigo kwa kuandika waraka mrefu bila kumtaja Hamisa lakini wapenda ubuyu wakatafsiri kuwa ujumbe umefika. Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na mgogoro kati ya Hamisa na Lulu huku madai ya msingi yakiwa ni kitendo cha Lulu kumchukulia Hamisa baba mtoto wake.

Chanzo:GPL

Baada ya kuoa mwanamke mwingine, Isabella adai ni yeye ndiye alimpiga chini Kalama, adai ni mwanaume asiye na future

Baada ya rapper wa kundi la Gangwe Mobb, Luteni Kalama kuoa mwanamke mwingine na kumwacha mchumba wake aliyemvisha pete, Isabella ameibuka na kudai kuwa ni yeye ndiye aliyemwacha baada ya kumuona ni mwanaume asiye na future.

“Mimi na Kalama tulikuwa tumeshaachana muda mrefu kwasababu nimeona ni mwanaume ambaye hana future hawazi chochote, kwahiyo nikaona kwanini nijipotezee muda. Mwanaume anaamka saa saba, kwahiyo nikaona niachane naye,” Isabela alimuambia mtangazaji wa Jembe FM, Natty E.

“Lakini watu wameona ilivyotokea gazeti wanahisi labda Kalama aliniacha mimi kitu ambacho sio kweli, hana uwezo wa kuniacha, mimi ndio nilimuacha. Na nafikiri stress zake ndio zimemfanya aende akamuoe rafiki yangu sasa si ni uchizi. Halafu mwanamke unaoa unaenda kukaa kwa mwanamke tena, yeye si ndio anakuwa ameolewa, kwahiyo yeye ni mwanaume ambaye ni kilaza,” aliongeza Isabela.

Wema Sepetu Adai Mwaka 2006 Ulikuwa Mwisho wa Miss Tanzania

Staa wa bongo movie,  Wema Sepetu ambaye pia aliwahi kuwa Miss Tanzania 2006 amesema hajui lolote kuhusu mashindano hayo zaidi ya kuwa mwaka alioshinda yeye ndiyo ulikuwa wa mwisho kwa mashindano hayo.

Hawa ndiyo walikuwa washindi watatu wa Miss Tanzania 2006,kulia ni Lisa (Mshindi wa 2),Kati ni Wema Sepetu (Mshindi wa 1) na Jokate (Mshindi wa 3).
Hawa ndiyo walikuwa washindi watatu wa Miss Tanzania 2006,kulia ni Lisa (Mshindi wa 2),Kati ni Wema Sepetu (Mshindi wa 1) na Jokate (Mshindi wa 3).
Mwaka jana mashindano ya Miss Tanzania yalifungiwa na BASATA kutokana na tuhuma za upangaji wa matokeo uliosababisha kupoteza msisimko na mvuto wa mashindano hayo. Hata hivyo mashindano hayo yamerejea tena.

Akiongea na Times FM, Wema alisema, “Sijui ni nini hasa kimetokea, maana mimi sifuatilii kabisa Miss Tanzania kwa sasa wala sijui Miss Tanzania mwaka huu anaitwa nani, nimeamua kuachana nayo kabisa sijui lolote, ila ninachojua mimi 2006 ndio mwaka wa mwisho wa Miss Tanzania.”

Bongo5

MUHIMU: FAHAMU NAMNA YA KUJITAMBUA JINSI ULIVYO


Siku moja niliona kwenye televisheni mahojiano kati ya mtangazaji na kiongozi mmoja mashuhuri katika nchi fulani. Wakati huo katika nchi hiyo Uchaguzi Mkuu ulikuwa umekaribia.
Hivyo, mtangazaji alimuuliza yule kiongozi kama alikuwa akitarajia kugombea urais wa nchi hiyo kwa kuwa aliyekuwa madarakani alikuwa anamaliza kipindi chake.
Yule kiongozi alimwambia mtangazaji kuwa yeye ana tabia ya kujitazama kwenye kioo kila siku asubuhi kabla hajatoka nje. Aliendelea kusema kuwa siku zote anapojitazama kwenye kioo hajawahi hata mara moja kujiona kuwa yeye ana wajihi unaofaa kwa kuwa rais.
Yule mtangazaji alipomwuuliza yule kiongozi anawezaje kwa kujitazama tu kwenye kioo kutambua kama anafaa au hafai kuwa rais, alielezea habari nyingine hadi muda wa kipindi ukaisha bila kujibu swali hilo.
Je wewe unajitambua jinsi ulivyo? Je unapochukua kioo ukajitazama unaweza kujitambua wewe ni mtu wa namna gani au unaweza tu kutambua jinsi sura yako ilivyo. Nasita kusema kama kioo kitakaonyesha jinsi sura yako inavyoonekana kwa kuwa watu wanaweza kutofautiana kwa jinsi wanavyoiona sura yako. Labda nikuulize swali jingine je kwa kujitazama kwenye kioo unaweza kupata viashiria vya mabadiliko unayostahili kuyafanya ili uwe mtu tofauti na ulivyo sasa. Sijui jibu lako litakavyokuwa kuhusu jinsi unavyoweza kukitumia kioo kikusaidie kujitambua, lakini mimi nimejaribu mara nyingi kujitazama, lakini hakikuweza kunisaidia kujitambua jinsi nilivyo.
Kitu kimoja muhimu zaidi kuliko vyote katika maisha ya binadamu ni kuwa na tabia nzuri na inayowapendeza na kuwavutia watu. Tunapokuwa watoto wazazi, walimu na jamii hujitahidi kutufunza mienendo mizuri na tabia njema.
Hata hivyo, kadri tunavyokua kuna baadhi ya tabia huziacha na pengine kuongeza nyingine. Bila kujali mchanganyiko wa tabia tunazokuwa nazo tunapokuwa watu wazima, wajibu wa kuhakikisha tunakuwa na tabia na mwenendo unaofaa katika jamii unakuwa mikononi mwetu.
Je tunaweza kushika hatamu za mienendo yetu. Hatuna budi kujitambua jinsi tulivyo na namna tunavyoonekana kwa watu wengine. Aidha, tunalazimika kubaini kama kuna mambo dhaifu tunayostahili kuyabadili ili tuwe na tabia bora.
Hata hivyo, ni kitu gani kinaweza kutusaidia kujichunguza sisi wenyewe? Tunaweza kujichunguza kwa kutumia hisia binafsi. Mtu anaweza kutenda jambo fulani njiani wakati akielekea nyumbani. Anapofika anaweza kukaa peke yake akawaza na kusema na nafsi yake yeye mwenyewe “Jambo lile nililofanya halikuwa zuri. Sitarudia tena kufanya hivyo.” Kile kinachomfanya ajisahihishe yeye mwenyewe ndicho kinachoitwa hisia binafsi. Hii ndiyo inayomsaidia mtu kujitambua jinsi alivyo na hata kumfanya aweze kupeleka mawazo yake mbele na kubaini inafaa aweje baadaye. Kwa kuzingatia kanuni hii inambidi kila mtu kujenga au kuimarisha hisia binafsi katika akili yake ili aishi akijitambua wakati wote na kujirekebisha kila inapobidi. Wala tusiwe na mawazo yasiyo sahihi ambayo baadhi ya watu huwa nayo wakasema: “Nimechelewa muda umepita na sasa hakuna ninachoweza kufanya ili kubadili tabia yangu.”
Mwanafalsafa mmoja alisema maisha ya mtu ni kama kitabu. Kila siku anayoishi anaandika ukurasa mpya. Hawezi kubadili kurasa zilizopita, lakini anaweza kuhakikisha kila ukurasa mpya unaofuata anaufanya kuwa mzuri zaidi kuliko ule uliopita. Hivyo ndivyo inayobidi tuishi.
Tunawezaje kujenga au kuimarisha hisia binafsi zetu?
Tunajenga hisia binafsi kadri tunavyoishi na kuutambua ulimwengu kwa kutumia milango ya fahamu. Kwa mfano; kijana anapofua au kutupa nguo zake ovyo ovyo na akawasikia wazazi wake wakigomba na kusema: “Wewe ni mtoto mbaya hutakiwi kuzifanya nguo zako hivyo.” Wakati anapozifua, akazipiga pasi na kuzipanga sandukuni na kisha akawasikia wazazi wake wakisema: “Wewe ni mtoto mzuri kwa kuwa unatunza nguo zako.” Iwapo hali itaendelea vivyo hivyo na kijana akawa anasikiliza maneno hayo siku baada ya siku, mwezi hadi mwezi, na mwaka mmoja hadi mwingine hupata funzo kuu katika maisha. Nalo ni hili, yeye ni kijana mbaya anapofanya mambo mabaya na kujifanya asipendwe, lakini anapofanya mambo mazuri anakuwa kijana mzuri na anajifanya apendwe.
Pia kama kijana huyo njiani huwa anawapita watu waliokaa kwenye kibaraza cha nyumba yao bila kusema chochote hakuna lolote litakatokea. Lakini siku moja akiamua kuwasalimu watamwitikia kwa furaha. Baada ya hapo siku nyingine akipita hata kama atakaa kimya watu hao watamchangamkia na kumsalimu. Hapana shaka hilo litakuwa somo kwake kwamba wameunda mawasiliano ambayo yamewajengea mazingira rafiki.
Hivyo, ndivyo hisia binafsi inavyojengeka kutokana na mchanganyiko wa taarifa na mwitikio kutoka kwa watu wengine. Aidha, tunabaini kuwa hisia binafsi hujengeka kutokana na jinsi tunavyojifunza, kupata uzoefu na mrejesho tunayopata kutokana na watu wengine.
Tunawezaje kuamua jinsi tunavyotaka tuwe baadaye
Baada ya kujua jinsi tunavyo baki na changamoto ya kubadilika ili tuwe watu bora zaidi kuliko tulivyo. Kwa kutumia hisia binafsi tunaweza kutumia mbinu ya kuigiza watu wengine. Chagua mtu anayekuvutia sana katika maisha yako. Anaweza kuwa angali hai au amefariki. Orodhesha mambo yanayokufurahisha kutokana na jinsi ilivyo. Mtu mmoja alipoulizwa mtu anayemvutia sana katika maisha yake alimtaja Nelso Mandela. Alipoulizwa sababu ya kuvutiwa naye alisema kwa sababu alikuwa mtu aliyeheshimiwa na kupendwa kutokana na upendo wa dhati aliokuwa nao kwa watu na taifa lake. Alikuwa tayari kuteseka ili wengine wapate heshima, haki na uhuru.
Tunapozichunguza sifa za Mandela alizozitaja mtu huyo tunapata picha kuwa ndizo tabia anazozipenda katika maisha yake. Huenda baadhi ya hizo yeye anazo na kama hanazo angependelea awe nazo. Huu ndio mchakato wa mawazo ambao unaweza kumfanya mtu kuwa na hisia za jinsi ambavyo angependa awe.
Kutokana na niliyoyandika katika makala hii hatuna budi kufanya kila juhudi ili tuweze kujitambua jinsi tulivyo. Tunapojitambua tulivyo tunapata fursa ya kuboresha hali zetu ili tuwe watu bora zaidi.
Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top