Loading...

Ababu Namwamba BOYCOTTED Raila Rally in Busia, was Surprised with the TURNED UP to give CORD Brigade super reception

 Ababu Namwamba BOYCOTTED Raila Rally in Busia, was Surprised with the TURNED UP to give CORD Brigade super reception
By Kamasasa E
Good evening Hon Ababu Namwamba!
You have expressed yourself well. The point is home. Baba has refused to disown you. In his heart, you still remain his son. When your dad bypasses other siblings advises and opt to stick with you, its high time you swallow your ego and ship up.
Your expectations today as Raila was in Butula, Busia:
1. Raila should not get a mammoth crowd in Busia county>> well, the events were flooded by a sea of humanity, pole sana.
2. A few guys who appeared like your surrogates and may be had been given a few coins to disrupt Raila rally were badly silenced within a record of 10 seconds. They folded their tails and joined the wagon of cheering on Tinga.
3. That the media will be deployed to paint how Raila has lost ground in Busia county, well Raila is resurgent!
4. That Raila would back Governor Ojaamong and Women rep Hon Mutua re-election next year. This was your epitome of rebel. Tinga was wise, he stayed clear of 2017 campaigns for local leaders.
You will realize the contrary happened. The opposite occurred. It shows your strategy failed. It doesn’t mean the message has not reached home. NO! Its home. Now an experienced soldier knows when to retreat, surrender or soldier on with injuries.
Take the right step. Make a wise step. Put off a little few guys who are trying to confuse you with misplaced cheering. They will be the first to laugh at you when in a political cold jug. That crowd that welcomed Raila must sent a message to you that nobody in Busia county who can hold Raila at ransom. He enjoys direct grass roots support. If you didn’t have a clear picture of the rally, check yourself below photos.

'Bavicha threaten to block CCM handing over ceremony'

 
RETIRED President Jakaya Kikwete and the outgoing Chairman of CCM is expected to hand over the party’s chairmanship to President John Magufuli next month as the Party’s Central Committee (CC) announced last week.
Party spokesperson Christopher Ole Sendeka told reporters in Dar es Salaam that the handing over will be done at a one-day special general meeting scheduled for July 23 in Dodoma.
He said the handing-over date was agreed upon at a meeting of the Central Committee (CC) held at the party’s Mainland sub-head office in Dar es Salaam yesterday, under the chairmanship of Mr Kikwete.
But addressing a press conference here yesterday, BAVICHA chairperson Julias Mwita argued that they will block the meeting in the same spirit the police disrupted their meeting last week, saying the law enforcers are used to suppress democracy in the country.
He said the police is used to oppress the opposition party, denying them opportunity to conduct political meetings including last week incidence here where the police disrupted a graduation party organized by youths affiliated to the party.

Dr Mengi donates desks for schools in Handeni,Bagamoyo districts'

 
Handing over two dummy cheques to two district commissioners yesterday in Dar es Salaam, Dr Mengi said: “There is no way the country can succeed in fighting poverty without investing in education.”
“Whenever we speak about education, some people think that the one who receives it is the one who will benefit …This concept is not true because educating children the whole nation is going to harvest the fruits,” he said.
He underscored the need for the public to invest in quality education of the children as they are going to realise marvelous advantages in the future.
Dr Mengi also called upon well to do people to support the efforts and donate whatever they have to assist the children in the country learn in favourable environments.
“There are some people who have been blessed by God because their living good life, I call upon them to help improving the education sector and God will bless them more,” Dr Mengi explained.
He also promised to assist the two districts by holding desk fundraising events to make them abide by the president’s directive.

magufuli-tells-opposition-leaders-dont-stand-my-way'

 
Magufuli's remarks yesterday, at a State House function where he received the National Electoral Commission (NEC)’s official report on last year’s general election, came against the backdrop of growing criticism that his government is intent on cracking down on dissenting voices and freedom of speech.
But he asserted that it was time for petty politicking to be put on hold to allow his administration to go about keeping all the promises made to voters during the campaign period leading up to last year’s polls.
“I was voted to be the president of all Tanzanians and I promised to serve them, therefore I will not sit back and watch someone try to deliberately derail my efforts to do this over the five years of my mandate,” he said.
He added: "I would like to urge my fellow politicians to conduct their political business through the people's duly-elected representatives, using appropriate platforms such as parliament."
Leaders of the main opposition parties in the country recently disclosed plans to stage nationwide public rallies and demonstrations to call for broader democracy in the country.
The police then swiftly moved in to ban the planned rallies, saying they were aimed at causing civil disorder.

Hata Kuziba Midomo ni Demokrasia-Rais Magufuli

Akizungumza leo Ikulu Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amewataka wanasiasa waliopewa nafasi za uwakilishi na wananchi wajikite zaidi katika kuwahudumia ili kuwaletea maendeleo waliyowaahidi wakati wa kampeni.

Rais Magufuli amesema kuwa wakati wa uchaguzi umekwisha hivyo wakati wa siasa sasa nao umekwisha hivyo amewataka viongozi wao wa siasa kushirikiana nae katika kuleta maendeleo ikiwemo kumpa ushauri ambao nae ataufanyia kazi kwa maendeleo ya Wananchi wote.

Dkt. Magufuli amesema kuwa kamwe hatomvumilia mtu yoyote ambae atamchelewesha katika harakati zake za kuwaletea maendeleo wananchi, hivyo ni vyema wakaungana kwa pamoja katika kufanikisha suala hilo.

Rais Magufuli amesema wabunge waliochaguliwa waelekeze nguvu katika kuwasemea wananchi kwa kufuata demokrasia ingawa hata kuziba midomo ni demokrasia ya aina yake lakini amevitaka vyama vyote kushirikiana nae katika kulileta taifa maendeleo.

Risasi Zarindima Zanzibar ........ Watu watatu Wajeruhiwa

Watu watatu wamejeruhiwa kwa kupigwa risasi na askari wa vikosi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na kupelekwa hospitali ya Alrahma kwa matibabu.

Majeruhi hao ni Yussuf Ali Juma (23), Ali Shaame Ibrahim (18) na Salim Masoud Bakar (18), wakazi wa Tomondo Wilaya ya Magharibi Unguja.

Kabla ya watu hao kujeruhiwa, milio ya risasi ilitawala jana majira ya saa 8:30 mchana katika mitaa ya Tomondo, Mwanakwerekwe na Kilimani, hivyo kuzua taharuki miongoni wakazi wa mitaa hiyo.

Mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa waliyaona magari ya vikosi hivyo yakiendeshwa kwa mwendo kasi kuzunguka maeneo hayo huku yakiwa na askari wakifyatua risasi.

“Mimi kwa sasa nipo hapa Kilimani na hivi punde tu risasi tumezisikia kutokea upande huu wa Mwanakwerekwe na Jang’ombe na ghafla naona watu wanakimbizwa kuletwa hapa Alrahma” alisema Rashid Said (54), mkazi wa Migombani ambaye ni dereva teksi.

Majeruhi Ibrahim alisema: “Walikuja wale mazombi, wengine walifunika uso waliwafungua ng’ombe wetu na kutaka kuwachukua, kwanza wakapiga risasi juu, tulipoona wanawapakiza katika magari lao tukasogea ndipo wakatupiga risasi.”

Bakari Juma (35), mkazi wa Msheleshelini alisema: “Tunasikia hawa jamaa wanataka wauze kitoweo cha nyama siku za sikukuu peke yao, lakini miye nasema sawa wafanye hivyo, ila si kwa ng’ombe wa kupora.”

Baadhi ya wananchi walidai kuwa mifugo hiyo wakiwamo ng’ombe wa maziwa ni mali yao.

Mmoja wa wafugaji hao aliyejitambulisha kwa jina moja la Omar alisema: “Sisi tunafuga ng’ombe hawa kama mnavyoyaona mabanda yetu yapo si miaka kumi wala ishirini ni tangu zamani wakati huo Tomondo ni pori tupu na mpaka sasa mifugo yetu haizururi wala haimkeri mtu yeyote.”

Licha ya askari kudaiwa kufika eneo la tukio na katika hospitali walikolazwa majeruhi hao, hali ya usalama ilionekana kuyumba pale makundi ya watu yalipohamasika kusogelea maeneo hayo.

Waliofika katika hospitali hiyo ni pamoja na Mkurugenzi wa Habari na Mahusiano kwa Umma wa Chama cha Wananchi (CUF), Salim Abdalla Bimani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kufuatilia zaidi ili kubaini chanzo chake.

Hata hivyo, alisema polisi waliingilia kati na kwenda katika maeneo hayo kurejesha hali ya usalama.

“Sijapata kwa ukamilifu kilichotokea, lakini ni kweli hawa vikosi wanaendesha operesheni ya kukamata ng’ombe wanaozurura mitaani, wamekwenda huko na kukatokea kukwaruzana baada ya kuwepo vijana ambao hawataki kuondoa ng’ombe, nimepeleka askari kutuliza hali na sasa hali imekuwa ya amani”, alisema Kamanda Mkadam.

Magufuli apuuza donda la Wazanzibari

 John Magufuli, Rais wa Tanzania, akiteta jambo na Dk. Ali Mohamed Shein, Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM
RAIS John Magufuli amepuuza maalamiko ya Wazanzibar kwamba, Chama Cha Mapinduzi (CCM) licha ya kukataliwa, kimelazimisha kurudi madarakani, anaandika Mwandishi Wetu.
Amempongeza Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC), kwa kile alichosema “ametimiza wajibu wake wa kusimamia uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa mwaka jana vizuri.”
Kwa kauli hiyo ambayo Dk. Magufuli ameitoa leo kwenye hafla ya kukabidhiwa ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania uliofanyika mwaka jana, hajabadilisha msimamo kuhusu mgogoro wa kisiasa Zanzibar uliotokana na uchaguzi huo.
Rais Magufuli amesema, uamuzi alioufanya wa kupeleka Zanzibar askari wengi wa vikosi vya ulinzi na usalama kulinda ili uchaguzi wa marudio wa 20 Machi 2016 uwe wa amani na salama ulikuwa sahihi na kwamba, naye alitimiza jukumu lake kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Amesema, hakuna uchaguzi unaokosa kasoro hata ndogo lakini anashangaa kwamba, wapo watu wanahangaika mpaka nje ya nchi kuieleza vibaya serikali kwa kuwa, nilisema siwezi kuingilia tume ambayo ni huru.
“Ni kweli sina mamlaka ya kuingia Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ambayo ikifanya uamuzi haiwezi kuhojiwa lakini nilipochukua hatua za kuimarisha ulinzi, nilitimiza wajibu wangu,” amesema.
Hata hivyo amesema kwa kurudia kuwa, uchaguzi umwekwisha nchini na sasa ni wakati wa kuwatumikia wananchi katika maendeleo.
“Walewale waliokuja kunitaka niingilie maamuzi ya tume nikakataa wamekuwa wanaisema serikali ninayoongoza,” amesema bila kutajia jina la mtu huyo lakini alikuwa akimlenga Maalim Seif Sharif Hamada, Katibu Mkuu wa CUF.
Maalim Seif yupo ziarani nchini Marekani, Canada ambapo amekuwa akieleza hali halisi ya uchaguzi wa Zanzibar namna ulivyovurugwa na Serikali ya CCM kwa lengo la kuendelea kubaki madarakani.
CUF chini ya Maalim Seif anayejinasibu kuwa ndiye rais wa Zanzibar aliyechaguliwa kihalali na wananchi, kinapinga uamuzi wa Jecha kufuta uchaguzi uliofanyika Zanzibar tarehe 25 Oktoba 2015 kwa kuwa, hakuwa na mamlaka ya kisheria ya kufanya hivyo.
Jecha alifuta uchaguzi huo tarehe 28 Oktoba 2015 kwa madai uliharibika na kisha kusimamia ualioitwa uchaguzi wa marudio wa tarehe 20 Machi 2016.
Baada ya uchaguzi huo Jecha alimtangaza Dk. Shein, mgombea wa CCM kuwa mshindi wa urais.

Sangoma wapandishwa kortini

 Jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
WATU watatu wanaosadikika kuwa waganga wa kienyeji wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa la kosa utapeli, anaandika Faki Sosi.
Watu hao ni Halid Mjewa (55), Salum Mwawala (24) na Said Magand (28).
Akisoma mashtka hayo Nassoro Katuga, mbele ya Magreth Bankika, Hakimu Mkazi katika mahakama hiyo amesema, kwa waakati tofauti mwaka 2012 katika eneo lisilojulikana kwa pamoja walijipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Katuga amedai kuwa, kati ya mwezi Januari hadi Desemba 2012 eneo la Kibamba, Kinondoni jijini Dar es Salaam walidanganya na kijipatia kiasi cha Sh. 260 milioni kutoka kwa Sophia Lolila kwa kujifanya waganga na kudai watamsaidia kwa nguvu za giza aolewe, kupata watoto na biashara yake ya mbao itaenda vizuri.
Katuga amesema kuwa, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kwamba, kesi hiyo itajwe kwa usikilizwaji wa awali.
Washtakiwa wote wamekana mashitaka hayo. Dhamana ya washitakiwa ipo wazi kwa mashrti ya kila mmoja awe na wadhamini wawili na kusaini hati ya dhamana ya Sh. 43.3Milioni kila mmoja.Kesi itatajwa tena Julai 4 Mwaka huu.

BREAKING NEWS: ZITTO ZUBERI KABWE FOR ANOTHER TIME ATTACK PRESIDENT MAGUFULI FOR THIS NECCESARY ISSUE WHICH ARE COUNTIUE IN TANZANIA

 John Magufuli, Rais wa Tanzania (kulia) akisalimiana na Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo
ZITTO Kabwe, kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo ametoa tamko lake juu ya kauli ya Rais John Magufuli ya kupiga marufuku vyama vya siasa kufanya shughuli za kisiasa zaidi ya bungeni na kwenye kampeni za mwaka 2020 ni sawa na kuua demokrasia.
Kwa habari zaidi soma tamko la Zitto Kabwe juu ya kauli hiyo hapa chini. 
Kauli ya Rais John Magufuli kuzuia yyama kufanya Siasa mpaka mwaka 2020.
Tumepokea kwa MSHTUKO na masikitiko makubwa kauli ya Rais kwamba vyama vya siasa havipaswi kufanya siasa isipokuwa wakati wa kampeni na kupitia bungeni.
Tunaichukulia kauli ya Rais kama tangazo la vita dhidi ya demokrasia na uhai wa vyama vingi nchini. Chama chetu kitaitisha vikao vya dharura kujadili hali ya nchi na namna ya kukabiliana na mashambulizi yanayoendelea dhidi ya demokrasia nchini mwetu.
Tunatoa wito kwa vyama vyote vya siasa nchini kuunganisha nguvu katika kuhakikisha tunapigana vita hii pamoja. Huu ni wakati wa vyama vya siasa na wanasiasa kuacha tofauti zao na kupambana kulinda uhuru wa kufanya siasa wakati wowote kwa mujibu wa Sheria.
Tunatoa wito kwa wananchi wote na taasisi za kiraia kusimama imara katika kulinda demokrasia. Tunasisitiza kuwa ushahidi wa kisayansi unaonyesha kuwa huwezi kuua demokrasia bila kuua juhudi za maendeleo. Tusiruhusu mtu yeyote mwenye mamlaka kuua demokrasia nchini mwetu.
Hatua zozote za kuua demokrasia ni kuua Umoja, Amani na mshikamano wa wananchi na Taifa, ambayo ndiyo msingi wa maendeleo ya nchi yetu kijamii, kisiasa na kiuchumi. Tunatoa wito kwa wananchi wote kushikamana na kusimama imara katika kulinda demokrasia.

BREAKING NEWS: THE NEW STYLE OF UKAWA WHICH INTRODUCE IN PARLIAMENT ARE TRANING IN SOCIAL NETWORK.....

 
Dar es Salaam. Picha za watu wa kada mbalimbali nchini wakiigiza ‘staili’ mpya ya wabunge wa Ukawa waliojibandika karatasi midomoni zenye ujumbe tofauti kuhusu haki ya uhuru wa Bunge wanayodai kuminywa na Naibu Spika, Dk Tulia Ackson zimeiteka mitandao ya kijamii nchini.
Tukio la wabunge hao lilitokea juzi mjini Dodoma ikiwa ni mwendelezo wa siku 17 za kususa vikao vinavyoongozwa na Dk Tulia tangu akatae kujadili hoja ya kusimamishwa wanafunzi 7,802 wa stashahada maalumu ya sayansi katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), wiki tatu zilizopita.
Kama ilivyokuwa kwa wabunge hao, watu mbalimbali wanapiga picha za kuigiza tukio hilo na kuziweka katika mitandao ya facebook, twitter na Instagram, baadhi wakiandika ujumbe kwenye karatasi wanazobandika midomoni ama wakiwaponda Ukawa au wakiwaunga mkono.
Mbali na waliobandika karatasi midomoni, wengine waliamua kujiziba kwa nguo, vilemba huku baadhi wakitumia kadi za CCM na Chadema na kuweka ujumbe wa kukosoa au kupongeza tukio hilo huku wengine wakitumia neno ‘kuziba mdomo’ kutoa yao ya moyoni ambayo hayahusiani na kitendo cha wabunge wa Ukawa.
Tukio hilo lilivuta wafuatiliaji wengi katika mitandao hiyo, katika ukurasa wa facebook wa gazeti hili @MwananchiNews, watu 255,372 walifungua picha za wabunge hao wa Ukawa huku watu 922 wakizinakili na kuzituma katika kurasa zao za mtandao.
Mbali na kuzifuatilia, wengine kwa mamia walikuwa wakitoa maoni yao yakieleza hisia mbalimbali.
Hali kama hiyo pia ilijitokeza katika tovuti ya Milladayo ambako watu 255 walitoa maoni yao katika picha hizo huku wakilumbana vikali.
Mkazi wa Dar es Salaam, Hilda Newton katika ukurasa wake wa facebook aliweka picha yake iliyoambatana na ujumbe unaosema ‘mkuu wa kaya acha kutuziba midomo na kukandamiza uhuru wa kuongea’.
Shija Steven katika ukurasa wake wa mtandao huo wa kijamii aliweka picha ya wabunge hao na kuponda kitendo walichokifanya, huku akiwashauri kwenda majimboni kutatua matatizo yanayowakabili wananchi.
Evelyne Ngoyai Meena katika ukurasa wake wa facebook aliandika, “kama mnafanya mambo mazuri kwanini hamtaki watu waongee, uhuru wa kujieleza uko wapi? Yanayoendelea nchi hii ni sawa na kufanya mtihani halafu unataka ujisahihishie mwenyewe.”
Picha za mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa katika ukurasa wake wa facebook zinazowaonyesha wabunge hao, zilijadiliwa na watu 7,971 huku watu 822 wakizinakili na kuziweka katika kurasa zao.
Katika ukurasa wake wa twitter, Papa Mchoyo aliweka picha ya mtu aliyejiziba mdomo kwa karatasi iliyoandikwa, “wabunge Ukawa achene maigizo.”
Kwa upande wake, Rev Mimba katika mtandao wa twitter aliandika, “tusiwabeze wabunge wa upinzani kuziba midomo katika political tactics (mbinu za kisiasa) za kufikisha ujumbe mbali na hiyo ni mojawapo.

Muhimbili yaboresha Huduma ya Chakula kwa Wagonjwa, Yawaondolea usumbufu ndugu wa wagonjwa kupeleka chakula mara tatu kwa siku.

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imeboresha huduma za chakula kwa wagonjwa wote watakaolazwa kuanzia Julai Mosi, mwaka huu ili kuwaondolea ndugu wa wagonjwa usumbufu na gharama za usafiri wakati wa wanapokwenda kuwaona ndugu zao waliolazwa mara tatu kwa siku katika hospitali hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana Jijini Dar Es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma, Hospitali ya Taifa Muhimbili Bw. Aminiel Aligaesha alisema hospitali imeingia ubia na mzabuni ili kutoa huduma hiyo kwa wagonjwa wote wanaolazwa.

Kwanini Hospitali imechukua hatua hii
Bw. Aligaesha alisema Hospitali inataka kujikita katika majukumu yake ya msingi ambayo ni kushauri, kuchunguza na kutibu.

“Aidha Hospitali inataka kuwaondelea adha ndugu wa wagonjwa ambao wamekuwa wakiingia gharama kubwa hususani usafiri wa kuja Hospitalini mara tatu kwa siku, ambapo kwa kukadiria gharama ya usafiri wa ndugu mmoja wa mgonjwa ni kati ya shilingi 6,000/= na 10,000/= kwa siku, kulingana na mahali anapotokea bila kujumuisha gharama za kuandaa chakula cha mgonjwa ambacho mara nyingi ni chakula maalumu.

"Na kama mgonjwa akilazwa zaidi ya siku tano hadi 10 ndugu mmoja wa mgonjwa gharama atalipia fedha nyingi kwenye usafiri” alisema Bw. Aligaesha

Aliongeza kuwa adha ya pili wanayopata ndugu ni usumbufu ambapo inabidi kuacha shughuli nyingine za uzalishaji ili kuja kuleta chakula mara tatu kwa siku, hivyo kuingiliana na shughuli zao za kiuchumi na kimandeleo na kushindwa kuzalisha. Hivyo jukumu hili linachukuliwa na Hospitali kuwaondolea adha hii.

“Pia kuna baadhi ya ndugu wamekuwa wakishindwa kuwaletea chakula wagonjwa wao hivyo hospitali ililazimika kuwapatia chakula ambacho kilikuwa kwa ajili ya wagonjwa wanaotoka mikoani wasio na ndugu hapa Dar Es Salaam” alisisitiza Bw. Aligaesha.

Alisema kumekuwepo na ongezeko la msongamano wa watu ndani ya Hospitali toka asubuhi saa 12 mpaka saa 12 jioni, suala linaloingiliana na utoaji huduma hasa saa za mchana kwani muda wa saa 6.00 hadi saa 8.00 mchana ulikuwa unaingiliana na majukumu ya kiutendaji ambapo majopo mbalimbali ya watalaamu yamekuwa yakiendelea na raundi za wagonjwa waliolazwa. Hii wakati mwingine imesababisha mgonjwa kutokupata huduma stahiki kutokana na muingiliano huu.
·                  
“Vile vile msongamano huu ni changamoto kwa ajili ya masuala ya kiusalama ambapo kati ya watu wanaoingia Hospitali kwa kigezo cha kuja kuona wagonjwa kuna wanaoingia kwa lengo la kufanya uhalifu ikiwemo wizi wa mali za Hospitali, magari  pamoja na vifaa vya magari” alisisitiza.
           
Alisema kwa kufanya hivyo, Hospitali itapunguza baadhi ya gharama za uagizaji wa vyakula kwa wazabuni, kulinda upotevu na baadhi ya vyakula kuharibika wakati mwingine kwani utunzaji wa vyakula una mahitaji makubwa.

Bw. Aligaesha alisema Hospitali inakusudia kutoa chakula chenye ubora na viwango vinavyotakiwa kwa wagonjwa ikiwemo kutoa chakula maalumu (special diet) kwa wagonjwa wenye uhitaji huo.

Utaratibu wa chakula cha mzabuni kwa wagonjwa
Kuhusu utaratibu huo Bw. Aligaesha alisema Mzabuni ndiye atakayepika chakula kwa wagonjwa wote waliolazwa na atatayarisha, atakipeleka na kukikabidhi katika wodi husika ambapo jukumu la kumpa mgonjwa kifungua kinywa, chakula cha mchana na jioni linabaki wa Hospitali.

Alisema wagonjwa watapatiwa milo mitatu kwa siku yaani asubuhi, mchana na jioni kazi itakayofanywa na muuguzi wa zamu ambaye atahakikisha wagonjwa wote wamepata chakula kufuatana na mahitaji (diet list) iliyowasilishwa jikoni kutokana na mahitaji yao ya kiafya.

Muda wa kuona wagonjwa
Kutokana na uamuzi huu, utaratibu wa ndugu kuleta chakula kwa wagonjwa waliolazwa wakati wa mchana umefutwa na hivyo mchana hatutakuwa na nafasi ya ndugu kuja kutembelea wagonjwa. M

uda wa kutembelea wagonjwa utakuwa asubuhi saa 12 hadi saa moja kamili na saa 10:00 jioni hadi saa 12:00jioni ndipo ndugu wataruhusiwa kuingia ndani kuwaona ndugu zao waliolazwa. Katika muda huo ndugu ataruhusiwa kuja na chakula chochote anachofikiri atamuongezea mgonjwa wake kama matunda n.k

Uchangiaji huduma ya chakula
Bw. Aligaesha alisema mgonjwa aliyelazwa atachangia kiasi cha shilingi 50,000 atakapolazwa ambapo kati ya hizo, shilingi elfu 10,000 itakuwa ni gharama ya kumuona daktari (Consultation), shilingi elfu 10,000 ikiwa ni gharama ya kulazwa na bei ya chakula itakuwa shilingi elfu 30,000 sawa na shilingi elfu 6,000 kwa siku. Wastani wa mgonjwa kukaa wodini ni siku tano. Gharama hizo zinahusika kwa muda wote atakaokuwa amelazwa.

Kwa sasa Hospitali inatoa chakula kwa wagonjwa 650 ambao wamepata rufaa kutoka hospitali za nje ya mkoa wa Dar es Salaam kwa gharama wastani wa shilingi 1.8 bilioni kwa mwaka, sawa na shilingi 150 milioni kwa mwezi kwa vyakula pamoja na  gharama nyingine kama vile za nishati.

Takribani wagonjwa kati ya 600 na 700 ambao rufaa zao ni kutoka Hospitali za Dar es Salaam walikuwa hawapati chakula kutoka Hospitalini, na ilibidi ndugu zao wawaletee chakula. Hata hivyo, Hospitali ilikuwa inawapatia chakula tu kama ndugu zao wakishindwa kufanya hivyo.

Hitimisho.
“Uongozi wa Hospitali unaamini kwamba mabadiliko haya hayatamuongezea mgonjwa gharama, bali yatampunguzia gharama pamoja na ile adha kama ilivyoainishwa hapo juu. Aidha, uongozi unaamini kwamba uamuzi huu unaendana na azma nzima ya kuboresha utoaji huduma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kuboresha mazingira ya Hospitali. Tunaomba ushirikiano wenu katika kutekeleza jukumu hili ili kusudi wagonjwa waweze kuhudumiwa vizuri zaidi” alisisitiza Bw. Aligaesha.

Mtoto wa Ajabu Mwenye Vichwa Viwili Azaliwa Geita


WANANCHI katika kijiji Kaseke kata ya Kasami wilayani na Mkoani Geita wamekubwa na taharuki na wasiwasi mkubwa mara baada ya  Geresi Saidi( 20) Kujifungua mtoto wa kiume mwenye vichwa viwili vinavyofanana sura.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jumapiri majira ya saa sita usiku katika katika kituo cha afya katoro alikwenda kujifungua muda mfupi baada ya kupata uchungu.

Channel Ten ilifika kijiji hapo na kushudia viumbe hao huku mamia yawananchi kutoka kila kona  wakifika na kushudia  tukio hilo na hapa mashuhuda wakaeleza ilivyokuwa.

Baba mzazi wa mtoto huo Stefano Lugisha amesema pamoja na mke wake kujifungua mtoto huyo lakini  ana imani kama ni mipango ya mungu kama amavyoeleza.

Diwani wa kata hiyo Anderea Karamura pamoja na mwenyekiti wa kijiji Zakaria Rukas wamewataka wananchi wao kutoliusisha tukio hilo na imani za kishilina swara hilo.

Akiongea kwa njia ya simu mganga kitua hicho aliyempokea mama huyona kumzalisha  Peter Janga amedhibitisha kutokea kwa na kwamba uchunguzi wa kina unafanyika ili kubaini nini tatizo kwa mama huyo ambaye hiyo ilikuwa ni nzao ya kwanza na kuongeza kuwa kiumbe hicho kilipoteza maisha baada ya muda mfupi.

BREAKING NEWS: AGIZO LA MAGUFULI NGOMA NZITO

 
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi madawati 2,600 kwa shule za msingi 74 za umma wilayani humo, Mkurugenzi wa manispaa hiyo, John Wanga, alisema wilaya hiyo ina upungufu huo wa madawati na kwamba uongozi uko katika jitihada za kuhakikisha inakamilisha kwa wakati uliopangwa.
“Tatizo kubwa liko kwa shule za msingi ambazo zina wanafunzi 78, 227. Upande wa shule za sekondari tunao upungufu wa madawati 4,812 na haya 2,600 ndiyo yako tayari kwa ajili ya kukabidhiwa kwa shule husika,” alisema Wanga.
Aliongeza kuwa katika kuhakikisha wanatekeleza agizo la Rais kwa wakati, halmashauri inaendelea kuhamasisha wadau kwa ajili ya kutengeneza na kukamilisha kabla ya mwisho wa muda uliowekwa.
Kutokana na uharaka wa mahitaji ya madawati hayo, wilaya ya Ilemela iliamua kuratibu utengenezaji huo katika shule ya ufundi ya wavulana Bwiru na madawati hayo yanatengenezwa na wanafunzi kwa kushirikiana na mafundi kutoka nje ya shule.
“Kila dawati linatugharimu Shilingi 98,000 mpaka 100,000 ambapo vifaa na mahitaji yote yananunuliwa na uongozi wa Halmashauri. Wanaotengeneza ni shule na wao hutudai Sh. 15,000 kwa kila dawati,” alisema.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Manju Msambya alisema ametoa agizo kwa watendaji wote kukataza matumizi ya vifaa vya shule kinyume cha maelekezo ili kulinda miundombinu ya shule na kuwaomba wazazi wasipotoshwe kuhusu kuchangia maendeleo ya kitaaluma kwa watoto wao na shule kwa ujumla.
Alisema wilaya inatarajia kuandaa hafla ya uchangiaji wa madawati kwa kuwahamsisha wazazi katika kukamilisha kazi hiyo kwa kuwa asilimia kubwa ya fedha za kutengeneza madawati ni za mapato ya ndani ya halmashauri.
Naye Msitahiki Meya wa Halmashuri ya Manispaa ya Ilemela, Renatus Mulunga alisema madawati 2,600 yaliyokabidhiwa jana, yanatarajiwa kusambazwa kwenye shule 74 za msingi za umma wilayani na kata 19 za wilaya hiyo zinatarajiwa kupata madawati 139 kila moja.
“Tunaendelea kukarabati madawati, meza, na viti vibovu katika shule za msingi na sekondari na mpaka sasa madawati 799 katika shule za msingi yameshakarabatiwa na meza 1,358, viti 1,237 vinaendelea kukarabatiwa katika shule za sekondari,” alisema Mulunga

Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp"

Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais kwenye mtandao wa WhatsApp.

Hapa cha muhimu ni kujuwa sheria hii inafanya kazi, inakamata, inahukumu na kufunga wananchi. Tutumie lugha ya staha, vijana hamko salama kwenye fb, twitter na WhatsApp...sheria ya mitandao ipo na inazunguka kama Simba aungurumae akitafuta mawindo

BREAKING NEWS: THE HOT NEWS NAPE NAUYE ATHREATINING DEATH OF SOME PEOPLE IN CCM AFTER DOING THIS THINGS.....


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amesema wakati wa mchakato wa chama kurejesha imani kwa wananchi hali ilikuwa ngumu kwake hadi kufikia kutishiwa maisha na watu wasiojulikana.

Mbali ya watu hao kumpigia simu za vitisho nyakati za usiku, pia walikuwa wakimchafua kupitia mitandao ya kijamii lakini anamshukuru Mwenyezi Mungu alivuka salama na chama kimevuka salama.

“Tulipoanza kuzunguka kujenga chama nilitukanwa sana. Watu waliwekeza kunichafua. Watu hao niliokuwa nawanyooshea kidole hawakufurahishwa na hatua ile hivyo wakaweka mkakati wa kutaka kunifukuzisha ndani ya chama na ilifika hatua wakawa wananichafua katika mitandao ya kijamii.

"Nikaamua kujitoa huko mpaka leo hii nimeamua kujitoa katika mitandao na kubaki katika twitter pekee kwa kuwa unaweza kutambua mtumiaji,” alisema Nape.

Akizungumza  nyumbani kwake mkoani Dodoma, Nape ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi na ambaye aliteuliwa kwa mara ya kwanza kushika nafasi hiyo mwaka 2011 Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete alipounda sekretarieti mpya chini ya Katibu Mkuu, William Mukama alisema watu hao walifikia kudai yeye si mtoto wa Mzee Moses Nnauye.

Kamati Kuu chini ya Mukama ilipita mikoani na kaulimbiu ya kuvua gamba iliyoasisiwa na chama kwa lengo la kuwaondoa watuhumiwa ufisadi lakini iliondolewa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2012 ikaundwa mpya chini ya Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana.

Kukata vigogo
Katibu huyo wa uenezi alisema changamoto kubwa waliyokutana nayo katika mchakato wa kumpata mgombea urais ndani ya CCM ilikuwa kukata majina ya waliokuwa viongozi wa Serikali ambao walijitokeza kugombea nafasi hiyo.

Nape alisema kumpata mgombea wa kupeperusha bendera ya chama hicho kongwe ilikuwa kazi nzito baada ya viongozi mbalimbali wa juu wa Serikali ya Awamu ya Nne kujitokeza wakiwamo, aliyekuwa Makamu wa Rais Dk Gharib Bilal, Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda na aliyekuwa Jaji Mkuu Augustino Ramadhani.

Vigogo wengine waliowapa wakati mgumu CCM ni aliyekuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Awamu ya Tatu na Nne, Frederick Sumaye na Edward Lowassa, na mawaziri kadhaa lakini kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu waliweza kutimiza wajibu wao.

“Kuwaondoa viongozi waliokuwa madarakani ni sawa na kutafuna jongoo kwa meno lakini hatukutetereka na hatimaye tukapata majina matano ambayo nayo yalipigiwa kura na kupatikana jina la mgombea mmoja,” alisema.

“Ingawa vikao vilikuwa vya moto sana na kulazimika kukesha mpaka usiku, kila mmoja alipata nafasi ya kujadiliwa na kutendewa haki siyo kama ilivyovumishwa kuwa wagombea wengine hawakujadiliwa,” alisema.

Nape alisema katika chama chao kila mwanachama ana nafasi sawa hivyo haikuwasumbua kuangalia majina ya watu hao wala nyadhifa zao badala yake waliangalia sifa za mgombea mwenyewe ndani ya chama.

Alisema anashukuru Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Jakaya Kikwete kwa kuwa na kifua cha kuhimili vishindo na hiyo ndiyo siri ya kufanikisha mchakato huo kwa kuwa ni mtoto wa CCM hivyo ilikuwa rahisi kumkata yeyote kwani uzoefu wake ndani ya chama ulisaidia.

Nape alisema itachukua muda mrefu kupata kiongozi kama yeye lakini pia hawawezi kupuuza kazi iliyofanywa na Katibu Mkuu wa chama hicho Abdulrahman Kinana na wazee waliorekebisha mambo na kuvuka salama kwa kuwa hali ilikuwa mbaya.

Bunge laivu
Nape alisema suala la kuzuia kurushwa moja kwa moja kwa matangazo ya Bunge si lake na kwamba lilipitishwa na wabunge wenyewe.

“Mimi ni msimamizi wa Serikali. Watu wanapotosha, nilichofanya ni kulinusuru Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), kwa miaka 10 mfululizo Bunge lilishindwa kuwalipa fedha zao ambazo ni Sh4.5 bilioni kila mwaka.

“Hili liwe fundisho kwa wabunge, kuna vitu wabunge wanapitisha hawavijui baada ya muda wanaona madhara yake wanaanza kulalamika kumbe walivipitisha wenyewe...Suala la Bunge kuanzisha kituo cha televisheni pia walilipitisha wenyewe, leo hii Katibu wa Bunge anavyotumia fedha kama ingekuwa haipo katika bajeti wasingemwacha,” alisema.

Dira ya Mtanzania wapandishwa kortini

 Untitled-1
MAHAKAMA  ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewapandisha kizimbani, mhariri na mwandishi wa gazeti la Dira ya Mtanzania, Musa Mkama na Prince Newton kwa kosa moja la kuandika habari za uongo zilizoleta mtafaruku kwa jamii, anaandika Josephat Isango
Akisoma hati ya mashtaka leo mbele ya Hakimu Respicius Mwijage, Wakili wa serikali, Timon Vitalis na Hellen Mushi, alidai mahakamani hapo kuwa, mnamo Juni 20 katika eneo la Biafra Kinondoni, Jijini Dar es Salaam washtakiwa hao waliandika na kuchapisha habari za uongo katika gazeti la ‘Dira ya Mtanzania’ toleo la 424 la tarehe 20 hadi 26 ambazo zilisababisha hofu na mshtuko kwa jamii kwa kutoa taarifa za uongo kuwa ’ Kifaru cha kivita cha Jeshi la Wananchi(JWTZ), chaibwa.
Amedai kuwa kitendo hicho ni kosa kisheria na ni kinyume na sheria ya magazeti.
Wakili Vitalis amedai kuwa, upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na kuiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.
Hata hivyo, washtakiwa hao wamekana shtaka hilo na Hakimu Mwijage amewataka kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja atasaini bondi ya Sh milioni 5.
Washtakiwa hao wamekidhi masharti ya dhamana na Hakimu Mwijage ameahirisha kesi hiyo hadi Julai 5 mwaka huu itakapotajwa tena.
Hata hivyo, chapisho hilo hilo katika ukurasa wa mbele na wa pili lilichapa kwa maandishi makubwa meusi na mekundu taarifa iliyosema: ‘Mwakyembe atuhumiwa kutapeli Bil.2.’ ambayo yalimuudhi Harrison Mwakyembe, Waziri wa Katiba na Sheria.
Mwakyembe ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wanahabari Mjini Dodoma na kudaikuwa, chombo hicho kimekosa weledi na kimepotosha umma kutokana na chapisho hilo.
“Hii si mara yangu ya kwanza kutuhuma na baadhi  ya habari kwa sababu mbalimbali zikiwemo za kisiasa, napenda nikiri mbele yenu kuwa sijawahi, kushuhudia upotoshaji mkubwa na wa makusudi na uzushi uliopitiliza na chuki binafsi iliyo bayana kama ambavyo gazeti hili limefanya,” amsema Dk. Mwakyembe na kuongeza;
“Nina taarifa kuwa, wameuza sana magazeti; naambiwa print order (idadi ya nakala) yao imeongezeka na kwamba taarifa yao imesambaa kwenye mitandao ya jamii, hivyo dunia nzima inajua mimi nina tuhuma za wizi, za utapeli.”
Pia amesema, gazeti hilo lililendelea kuandika tena Juni 20 wiki hii kwa kuuthibitishia ulimwengu kuwa, “Dk. Mwakyembe ni tapeli na ushahidi wao mkubwa wametaja barua iliyowahi kuandikwa na Kampuni ya Power Pool mwaka 2010 na mimi kutumiwa nakala kwa mtanzdao (e-mail) wanayodai ni yangu. Kwa busara za gazeti hili, huo ni ushahidi tosha kuwa mimi ni tapeli.
“Gazeti hilo halina staha na miiko ya uandishi wa habari, kikosi chetu cha jeshi huko Kisarawe kilielezewa kama kikundi cha wahuni hivi kinachopiga wananchi hovyo hovyo, kinapiga risasi za moto hovyo hovyo hadi kumpiga mwananchi moja kiunoni.”
Wakati huo huo ametoa tahadhari kwa televisheni kutosoma magazeti yenye taarifa tata akitoa mfano wa habari zilizoandikwa na gazeti la Dira kwamba, kifari cha jeshi kimeibwa.
“Tutafungua kesi hii Mahakama Kuu ya Tanzania, tutawapa taarifa kila tunavyoendelea. Bado tunaangalia impact (athari) na kuhusika kwa vyombo vikubwa vya habari kama ITV na STAR TV kutangaza taarifa za magazeti tata bila uangalifu ili na wao tuwahusishe katika kesi hii,” amesema na kuongeza;
“Kesi hii, nina uhakika, itajenga msingi imara wa wajibu na uhuru wa vyombo vya habari Tanzania kwa muda mrefu ujao.”

POLISI WAMDUWAZA SUMAYE KWA HILI

 Frederick Sumaye, Waziri Mkuu Mstaafu
FREDERICK SUMAYE, Waziri Mkuu Mstaafu pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema ameshangazwa na unyongaji demokrasia unaofanywa kwa kiwango kikubwa nchini, anaandika Dany Tibason.
Ametoa kauli hiyo jana mjini Dodoma muda mfupi baada ya Jeshi la Polisi kutumia nguvu kutawanya wanafunzi na wanachama wa Chadema Vyuo Vikuu Mkoa wa Dodoma (CHASO) wakati wakifaya mahafali yao ya saba kwa ajili ya kuagana.
Amesema, kitendo cha serikali kulifanya taifa lisiwe na nafasi ya kukosolewa ni dalili mbaya ya udikiteta na kamwe haiwezi kufumbiwa macho.
Amesema, hakuna serikali yoyote duniani ambayo inaweza kukataa kusemwa kwani kiongozi bora na shupavu ni ule ambaye anasemwa na kusikiliza watu wanasema nini.
Sumaye ambaye alikuwa awe mgeni rasmi katika mahafari hayo ambapo amesikitishwa na kitendo cha polisi kuzuia mahafali ya wanafunzi hao kwa kuwa ni haki yao kuagana na kubadilishana uongozi.
Amesema, imekuwa ni aibu kwa serikali kuendesha nchi kwa matakwa ya mtu mmoja jambo ambalo amesema ni kujenga chuki kwa wananchi hata pale ambapo hapakuwepo na sababu.
Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Tanzania Zanzibar amesema, bado uongozi wa Chaso unafanya tathimini ya kuona ni jinsi gani ya kufanya taratibu juu ya Jeshi la Polisi kuwasababishia hasara wanafunzi hao.
Amesema, pamoja na jeshi hilo kuingilia mahafali hayo, bado wanafanya maandalizi ya kuhakikisha mahafari hayo yanafanyika ili vijana hao waweze kupata haki yao.
Mwalimu amesema, kwa sasa serikali inaogopa upinzani na kamwe nguvu ya upinzani haitaweza kupunguzwa hata kwa siku moja na badala yake inazidi kuimarika.
Lazaro Mambo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma amesema, sababu za kuzuia mahakafali hayo ni kutokana na kuwepo kwa taarifa za uvunjifu wa amani.
Hata hivyo amesema, licha ya kuwepo kwa taarifa hizo tayari Jordan Lugimbana, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alikuwa ametoa zuio la kuwepo kwa mikutano ya kisiasa katika mkoa huo.

Madiwani Misungwi Wakanusha Kumtetea Kitwanga

Baraza la madiwani Halmashauri ya Misungwi limesema halijawahi kutoa kauli ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba hawakuunga mkono uamuzi wa Rais Dkt. John Magufuli kumfuta kazi aliyekuwa Waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga.

Taarifa ya baraza hilo baada ya kikao imesema kwamba ''Sii kweli kwamba kuna tamko lolote tulitoa kuhusu kufukuzwa Waziri Kitwanga na wala hatuna uwezo huo, taarifa hizo zibezwe na kupuuzwa.''
Madiwani hao wamesema wanaungana mkono na kauli ya Rais Dkt. John Magufuli kuhusu hapa kazi tu hivyo uamuzi wake alioufanya hawawezi kupingana nao.

Aidha baraza hilo limesema kama kuna mtu alitoa kauli kwa niaba ya baraza hilo siyo sahihi kwani baraza hilo hutoa taarifa zinazohusu mambo yao kwa kutumia vikao maalumu.

NEWSPAPERS FOR TODAY

IMG_20160619_050521IMG_20160619_050051IMG_20160619_050011

Ukawa: CCM wanatuumiza

Charles Kuyeko, Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala (Ukawa) (Wakwanza), Edward Lowassa, aliyekuwa Mgombea Urais kwa tiketi ya Ukawa na Boniface Jacob, Meya wa Halmashauri ya Kinondoni (Ukawa)VYAMA vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vinalalamika kuhujumiwa na na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), anaandika Regina Mkonde.
Viongozi wa vyama hivyo wanaeleza kuwa, hujuma za kisiasa zinazoendelea kufanywa na baadhi ya viongozi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, zimeacha athari kubwa.
Na kwamba, hujuma hizo zimesababisha Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni kukosa msaada wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi.
Kauli hiyo imetolewa jana na Boniface Jacob (Chadema), Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Jacob amesema kuwa, hujuma hizo zinahusisha kuwazuia viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kwenda safari za nje ya nchi ambazo zinalenga kukutana na wafadhili kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye wilaya zao.
“Hali ya kimahusiano kati ya mameya wanaotokana na Ukawa na Serikali Kuu si mazuri hata kidogo, viongozi tumeamua tuhabarishe umma wa Watanzania kuwa, kuna hujuma za waziwazi zinazofanywa na wenzetu juu ya shughuli za mameya wa Kinondoni, Ilala na Jiji la Dar es Salaam,” amesema.
Jacob amesema kuwa, hivi karibuni Ubalozi wa Uturuki ulidhamini safari ya mameya kwenda Uturuki kukutana na wadau na wafadhili wa miradi mbalimbali ikiwemo wa ujenzi wa Chuo Cha Ufundi ndani ya Manispaa ya Kinondoni.
“Ubalozi huo ulikuwa umeshatoa kibali cha kusafiri (Visa) na kugharamia fedha za usafiri, malazi, chakula na gharama zingine zote, ambapo matayarisho tu yali gharimu kiasi cha Dola za Marekani 42,000 (Sh 88 milioni) kwa mameya wote wanne, mtendaji mmoja mmoja kila halmashauri,” amesema.
Anasema, fedha hizo zililenga pia kugharamikia  mikutano iliyotakiwa kuanza tarehe 16 Juni mpaka 19 Juni 2016 na kwamba, wafadhili na wadau wa maendeleo waliandaa mialiko ya wawekezaji na wafadhili kutoka sehemu mbali mbali za Uturuki.
“Wafadhili hao walitarajiwa kuja Makao Makuu ya nchi hiyo, Jiji la Instanbul ili kukutana nasisi kujadili miradi ya maendeleo lakini serikali imevunja safari hiyo,” amesema.
Amesema, kitendo hicho cha serikali kuwazuia kimesababisha manispaa za Jiji la Dar es Salaam kukosa fursa za maendeleo ikiwemo chuo hicho cha ufundi.
“Si mara ya kwanza kwa sisi mameya kuhisi kuhujumiwa na baadhi ya viongozi serikalini ambao kimsingi, sisi tuliamini uchaguzi umeshapita na kwamba kila mmoja wetu atampa mwenzake heshima inayostahili juu ya ajenda za maendeleo,” amesema na kuongeza;
“Ndiyo maana kama nilivyo sema hapo awali, tumekuwa kimya juu ya vikwazo vidogo vidogo ambavyo tulihisi ni hujuma.
“Lakini tukaamua kuwa kimya na wavumilivu lakini tunatambua kuwa ipo mikakati ovu mingi dhidi yetu, ya kutukwamisha tusifanikiwe kuleta Maendeleo ndani ya mkoa wetu na wilaya zetu,” amesema.
Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top