Loading...

TID amlalamikia Billnass, ‘sijapenda alikuwa akinibembeleza nimsaidie ajulikane’


Msanii wa muziki na Mkurugenzi wa kundi la Radar Entertainment, TID ameingia kwenye mgogoro na rapper Billnas aliyekuwa member wa kundi hilo kabla ya kutimkia katika label mpya ya ‘LFLG’.

Mapema mwaka huu Billnas aliiambia Bongo5 kuwa aliondoka Rada bila matatizo na mtu yeyote.

Akiongea na Clouds Fm, TID amedai Billnass amesahau alikotoka na hatoi heshima kwa watu walio msaidia kumfikisha hapo alipo sasa.

“Mi sijapenda alikuwa akinibembeleza nimsaidie ajulikane, alikuwa ana nidhamu lakini sasa hivi hanipigii simu, tukimwambia afanye hivi hataki,” alilalamika TID. “Why do we help people who do not help us, why he think he is on top all over the sudden no!! People don’t live like that… People need to respect the people who help u… And of the day,”

Aliongeza, “Mimi i gave out to my heart, my voice, my energy, my talent to make him shine but I don’t see any effort, hajanipa hata laki moja kuniambia nashukuru, anafanya tour hata kuniambia Mzee Mnyama chukua hii laki tano umenifanyia chorus kali neve, huyo mtu wa aina gani hata ungekuwa wewe usingefurahi basi hata shilingi elfu kumi. The first time mimi ndiye niliyemleta Clouds Fm kufanya interview ananiambia siwezi kuongea anatetemeka, ningetaka kumsign halafu ningemmaliza ingekuwa kila napokwenda kufanya shoo angekuwa ananilipa lakini niliona kwamba sina shida kitu nilichokuwa nakihitaji ni ‘appreciation’ ndo maana watu wanatoa cirtificate of ‘Appreciation’,”

Kwa upnde wa Billnas akizungumzia issue hiyo alisema kuwa ameichukulia kawaida kauli hiyo na hajamkimbia TID.

“Mimi natambua mchango wake na nimewahi kuzungumza mara nyingi na najua nafasi yake kwangu na sijawahi kumdharau na kuondoka Radar halitakiwi liwe kosa,” alisema Billnass.

ZariTheBossLady Amtaja Ivan kwenye Post Moja na Diamond Platnumz

Kwenye siku ya BABA duniani wasanii tofauti wameonyesha ukaribu wao kwa watoto na familia zao kupitia instagram na mitandao tofauti ya kijamii.

Couple inayopewa attention kubwa kwa sasa bongo ya Zari na Diamond imechukua nafasi kubwa leo kwenye mitandao baada ya Zari kumtaja Ex wake ambaye ni Ivan [Baba wa watoto watatu wa Zari] kwenye post moja na Diamond Platnumz kitu ambacho hakijawahi kutokea.

Zari aliandika hivi 
"God has his timing for everything and he knows better why he does things at his own time. I know u felt this day would never come in your life but with God, NOTHING IS IMPOSSIBLE. Happy father’s day to you @diamondplatnumz and to the rest of the dads playing great roles in thier kids lives @ivandon. Happy father’s day to all women out there playing both roles"

Ray C Apelekwa Sober house Bagamoyo, Uongozi wa Sober Wazungumzia


Muimbaji mkongwe wa muziki nchini, Rehema Chalamila ‘Ray C’ Ijumaa hii amepelekwa Life and Hope & Rehabilitation Centre (Sober House) iliyopo Bagamoyo kwa ajili ya kusaidiwa kuanacha na matumizi ya Madawa ya kulevya, uongozi wa sober hiyo umethibitisha.


Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja toka aonekane katika video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii ikionyesha jinsi anavyosaidiwa na jeshi la polisi baada ya kudaiwa kutaka kijichoma kisu.


Mmoja kati ya wasimamizi wa kituo cha Life and Hope & Rehabilitation Centre (Sober House) ambacho pia kilimsaidia Chidi Benz kuachana na matuzi ya Madawa ya kulevya, Karim Banji, amesema kuwa ni siku moja toka Ray C apelekwe katika kituo hicho.


“Kweli jana tumempokea Ray C, na kusema kweli kwa sasa siwezi zungumzia maendeleo yake kwa sababu ni siku ya kwanza, lakini leo mchana amekula vizuri na nimemuacha amepumzika,” alisema Karim.


Pia alisema bado hajajua Ray C atakaa kwa muda gani ndani ya sober house.


“Kusema kweli mgonjwa akiletwa hapa, atapimwa afya na baada ya hapo anawekwa katika chumba maalum kwa siku tatu ili aweze kukabiliana na hali ngumu, na baada ya hapo ataendelea na matibabu ya kawaida, kwa hiyo kikubwa ni kuombea tu,” alisema Karim.

Mimi ni mwanamuziki, Shilole ni mcheza shoo – Nuh Mziwanda

Msanii wa muziki, Nuh Mziwanda ameendelea kumponda aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kwa kudai sio mwanamuziki bali ni mcheza shoo.
nuhu

Muimbaji huyo wa wimbo ‘Jike Shupa’ amekuwa akitupiana maneno na Shilole kupitia mitandao ya kijamii toka wimbo huyo utoke.

Akiongea katika kipindi cha The Base kinachoruka katika runinga ya ITV, Nuh alisema hawezi shindana na Shilole kwa kuwa sio mwanamuziki.

“Mimi sitaki kiki, mimi mambo ya kiki nimeshayaacha, sasa hivi na fans base kwa ajili ya Jike Shupa,” alisema Nuh. “Ila yeye (Shilole) anajaribu kunichokonoa ili maisha yake yaende. Mimi ni mwanamuziki babu, siwezi kushindana naye, yule ni mcheza shoo,”

Shilole na Nuh hawakuachana vizuri, kila mmoja amekuwa akimtupia maneno machafu mwenzake.

Mimi ni mwanamuziki, Shilole ni mcheza shoo – Nuh Mziwanda

Msanii wa muziki, Nuh Mziwanda ameendelea kumponda aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kwa kudai sio mwanamuziki bali ni mcheza shoo.
nuhu

Muimbaji huyo wa wimbo ‘Jike Shupa’ amekuwa akitupiana maneno na Shilole kupitia mitandao ya kijamii toka wimbo huyo utoke.

Akiongea katika kipindi cha The Base kinachoruka katika runinga ya ITV, Nuh alisema hawezi shindana na Shilole kwa kuwa sio mwanamuziki.

“Mimi sitaki kiki, mimi mambo ya kiki nimeshayaacha, sasa hivi na fans base kwa ajili ya Jike Shupa,” alisema Nuh. “Ila yeye (Shilole) anajaribu kunichokonoa ili maisha yake yaende. Mimi ni mwanamuziki babu, siwezi kushindana naye, yule ni mcheza shoo,”

Shilole na Nuh hawakuachana vizuri, kila mmoja amekuwa akimtupia maneno machafu mwenzake.

Video:Riyama Ally Afunga Ndoa na Leo Mysterio

Msanii wa filamu Riyama Ally Alhamisi hii amefunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu Leo Mysterio.

Muigizaji huyo mahiri wa filamu ambaye ni mama wa mtoto mmoja aliyezaa mume ambaye aliaacha naye, ameingia katika list ya wasanii wachache wa filamu waliofunga ndoa.

Leo Mysterio ambaye ni msanii chipukizi wa muziki, aliwahi kusema kuwa mahusiano yake na staa hiyo wa filamu, yalianza mwaka mmoja uliyopita.
Ndoa hiyo ilihudhuriwa na mastaa mbalimbali wa filamu.

Peter Msechu Akiri Mwili Wake Umemshinda...Anatafuta Wakumpa Stress


Msanii Peter Msechu amefunguka na kusema kuwa yeye mwili wake umemshinda sasa maana amejaribu kila mbinu kupunguza lakini wapi upo pale pale na yeye mambo ya kusema afanye diet hawezi kwani hela ya kununu matunda ya elfu nne kila siku hana.

Peter Msechu amesema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio na kusema sasa amegundua kitu pekee kinachoweza kupunguza mwili wake si kufanya diet bali ni kupata stress tu, hivyo anatafuta mtu wa kumpa stress ili apungue.

"Mambo ya kusema nafanya diet mimi siwezi hizo hela za kununua matunda ya elfu nne kila siku mimi sina, sijui hela ya gym hamna, saizi mimi nataka stress tu ili nipungue maana kitambi hiki saizi kimekuwa na mazalia kama arobaini hivi" alisema Peter Msechu

Mbali na hilo Peter Msechu alisema kuwa katika wimbo wao mpya ambao wamefanya na Banana Zoro kwa asilimia kubwa umeandaliwa na Banana Zoro na kusema yeye yupo karibu na Banana Zoro kutokana na ukweli kwamba wanafanya muziki wa aina moja wa live, na kusema huo ndiyo muziki wa kweli na si muziki wa wasanii wengi wa bongo ambao wanabebwa bebwa na computer kwa kutengenezwa.

Mashabiki ‘Wamteka’ Mwamuzi Mechi ikiendelea


MASHABIKI wa timu ya Friends Rangers, jana Jumanne uvumilivu uliwashinda baada ya kuchukua maamuzi magumu ya ‘kumteka’ mwamuzi wa pembeni aliyekuwa akichezesha mchezo wao dhidi ya Misosi FC kwenye Uwanja wa Makurumla, Magomeni, Dar.

Mchezo huo wa hatua ya 32 Bora ya michuano ya Sports Extra Ndondo Cup, ulimalizika kwa Misosi kuibuka na ushindi wa bao 1-0 lilofungwa na Idd Selemani dakika ya 31.

Championi lililokuwepo uwanjani hapo, liliwashuhudia mashabiki hao dakika ya 80 wakimbeba mwamuzi huyo ambaye jina lake halikufahamika haraka kwa madai kuwa alikuwa akiionea timu yao.

Hata hivyo, mwamuzi huyo aliachiliwa na kurudi uwanjani kumalizia mchezo huo ambao muda mwingi ulitawaliwa na vurugu zilizokuwa zikifanywa na mashabiki wa Friends.

Idris Asema Wema Kutumia Tsh Milioni 4.8 kwa Ajili ya Nywele kwa Mwezi ni Hadhi yake

Baada ya mashabiki na wadau mbalimbali kujadili kauli ya Wema Sepetu ya kwamba anatumia Tsh 4.8 kwa ajili ya nywele zake kwa mwezi mmoja, mpenzi wake Idris Sultan amesema matumizi hayo yanaendana na hadhi ya mrembo huyo.

Aidha katika kauli nyingine ambayo Wema aliitoa mapema mwaka huu, alisema anatumia Sh 30,000 kwa ajili ya chakula kwa siku na kama atanunua na chakula cha mbwa wake huwa anatumia Sh 50,000 kwa siku.

Akiongea na Bongo5 wiki hii, Idris Sultan ambaye ni mshindi wa shindano la Big Brother 2014, amesema haoni tatizo kwa mpenzi wake huyo kuwa namataumizi makubwa kwa kuwa yeye mwenyewe ni mtafutaji.

“Kwa level yake anafaa, kila mtu na level yake,” alisema Idris. “Kwa hiyo nina maanisha kila mtu ana thamani yake, na kila siku hadhi ya maisha yake inapanda na pia anafanya kazi ndiyo maana anafikia katika level hiyo,”

Pia Idris alisema watu wanatakiwa kutambua kwamba jinsi uchumi wa mtu binafsi unavyokuwa basi pia na maisha yake hudabilika pamoja na muonekano.

Picha: Professor Jay atembelea ‘WCB’ ya Diamond, afurahishwa na uwekezaji uliyofanywa

Mbunge wa Mikumi ambaye ni msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop, Joseph Haule ‘Professor Jay’ Jumatatu hii alitembelea ofisi za WCB na kujionea uwekezaji uliyofanywa na rais wa label hiyo Diamond Platunmz.

Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Professor Jay amemsifia Diamond kwa uwekezaji aliyoufanya.

“Kikubwa kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Diamond kwa kuwa na mawazo mapana zaidi kwa sababu kiukweli kwa wasanii wengi wa Tanzania na Waafrika wengi tunaweza tukawa na kipaji lakini mazingira yetu ya kazi yanakuwa magumu,” alisema Professor.

Aliongeza, “Kwa mfano pale kwa Daimond jana nimeenda nimekuta kuna studio hapo hapo, pamoja na kurecord lakini pia anachumba ambacho amekitengeneza cha kutengeneza photoshoot. Lakini pia ana sehemu ya kufanya editing ya kazi zake na ana watu special ambao amewaajiri kwa ajili ya kazi hizo, hii ni hatua kubwa sana kwa msanii,”

Dully Sykes: Sioi Leo Wala Kesho, Hata Baba Yangu Hakuwahi Kuoa

Baada ya kupost picha akiwa na Mwana FA baada ya kuoa na kuandika maneno yanayoashiria naye hivi karibuni atafuata nyayo za Mwana Fa, Dully Sykes ameruka viunzi na kusema hana mpango wa kuvuta jiko leo wala kesho.

Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Dully amesema yeye kwake kuoa ni sawa na maji kufuata mkondo, kwana hata marehemu baba yake hakuwahi kuoa wakati wa uhai wake.

“Kila mtu ana mipango yake, maji hufuata mkondo, wewe nafikiri mzazi wako alioa, mi baba yangu hakuwahi kuoa”, alisikika Dully akielezea sababu ya yeye kutoamua kuoa mpaka leo.

Pamoja na hayo Dully amesema akiona kuna umuhimu na ikiwezekana ataoa, hivyo amewataka wadau wake wamuombee ili aweze kuwa na mawazo ya kuoa na kuwa na mke rasmi.

“Kama inawezekana naweza kuvuta jiko, na kama haitowezekana sitavuta jiko, kwa sababu sijafikiria bado, mniombee nipate mawazo ya kuchukua jiko, sio kwa vile FA amefanya basi ndo uone inawezekana, nina sababu zangu tu mwenyewe, nikikwambia ntakuvunja moyo kama umeoa wewe”, alisema Dully Sykes.

Akaunti ya Instagram ya Linah yenye Followers milioni 1.3 Yadukuliwa (hacked)

Akaunti ya Instagram ya Linah yenye followers milioni 1.3 imedukuliwa (hacked) Jumanne hii.

Tayari hacker huyo ameibadilisha jina akaunti yake na kuipa jina ‘suponzetrie’ huku akifuta picha zake zote alizoziweka mwaka huu.

Post ya mwisho inayoonekana sasa ni video ya tamthilia ya Empire aliyoiweka December 27, 2015. Haijulikani nini lengo la hacker huyo na kama ni wa hapa hapa Tanzania.

Linah anakuwa msanii wa hivi karibuni ambaye akaunti yake ya Instagram imedukuliwa. Miezi kadhaa iliyopita akaunti ya Shilole pia ilidukuliwa japo alifanikiwa kuirejesha.

“Jamani daaaah ndo kama hivyo watu washafanya yao pole kwa uwezo wa Allah itarudi,” Shishi amempa pole Linah.

Zaidi ya kujitangaza, miaka ya hivi karibuni akaunti za mastaa zimekuwa moja ya vyanzo vyao muhimu vya kipato na wale wenye followers wengi wamekuwa wakipata deals zenye hela nyingi.

Ni wazi Linah atakuwa kwenye wakati mgumu kwa sasa.

Watu Hawajui Sisi Tuna Picha ya Diamond na Ali Kiba Wakiwa Wanaongea – Babu Tale

Mmoja kati ya viongozi wa juu wa label ya ‘WCB’, Babu Tale amesema watu hawajui kama Ali Kiba na Diamond wakikutana wanazungumza kama kawaida.
dd

Amesema hayo baada ya weekend hii kuzagaa picha katika mitandao ya kijamii inayomuonyesha Babu Tale, Sallam, Ommy Dimpoz, Mwana FA pamoja Ali Kiba wote wakiwa na nyuso za furaha hali ambayo liibua maswali mengi kwa mashabiki.

Akiongea katika kipindi cha XXL cha Clouds Fm, Jumanne hii, Babu Tale amewataka mashabiki wa muziki kuamiani kwamba yeye pamoja na Diamond hawana tatizo na Ali Kiba.

“Unajua binadamu wanatakiwa kubadilika, huwezi ukatengeneza dhana sisi tuna matatizo hatuwezi hata kupiga picha, hatuwezi kukaa pamoja, hatujafikia hatua hiyo, sisi tunabishana kimuziki na tunatengeneza value ya muziki ili muziki wa Tanzania ukue,” alisema Tale.

Aliongeza, “Haimaanishi Diamond na Ali Kiba wakikaa hawaongei, watu hawajui kuna picha ambazo sisi tunazo Diamond na Kiba wanaongea wapo studio kabisa. Hata kama tukiamua kizipost hizo watu wangeanza kuzungumza zitu vingine, picha ni kitu cha kawaida. Katika hii picha ambayo inazungumziwa alianza kuitwa Mwana FA, akaitwa Omary, akaitwa Ali, tukaitwa mimi na Sallam, kama ningekuwa sitaki kukaa karibu na Kiba ningekimbilia moja kwa moja kwa na Sallam kwa sababu sisi ni wamwisho kuitwa,”

Diamond na Ali Kiba ni wasanii ambao wanadaiwa hawaelewani kitu ambacho kimekuwa kikikanushwa na pande zote mbili.

Ben Pol Afunguka 'Muungano wa Diamond Platnumz na Rich Mavoko Utaleta Mapinduzi Makubwa Kwenye Muziki'

Mkali wa wimbo ‘Moyo Mashine’, Ben Pol amefunguka na kuzungumzia hatua ya Diamond Platnumz kumsani msanii kubwa kama Rich Mavoko katika label yake WCB.

Akiongea na Bongo5 hivi karibuni, Ben Pol amesema hatua ya Diamond kuamua kumsaini Rich Mavoko katika label ya WCB, itafungua njia kwa wasanii wengine kuwa na moyo wa kusaidiana wenyewe kwa wenyewe.

Ni vizuri sisi kwa sisi tukaaminiana na kufanya kolabo kwenye kazi,” alisema Ben Pol. “Diamond ni mpiganaji na Mavoko ni mtu ambaye ana kipaji na mjanja mjanja, kwa hiyo muungano wao unaweza kuleta mapinduzi makubwa katika muziki,”

Pia muimbaji huyo amewataka wale wasanii wenye uwezo wa kuwasaidia wenzao wasisite, kwani hiyo ndiyo njia sahihi ya kuupeleka muziki wa Tanzania mbele zaidi.

Mwanamuziki Linah Sanga Aweka Hisia zake za Mapenzi Kwa Mwanamuziki Darasa..Adai Anatamani Kuzaa Naye

Linah amesema anatamani kuzaa na mwanaume mwenye sifa kama za rapper Darassa.

Muimbaji huyo amesema kwa jinsi ambavyo amewahi kukaa na Darassa na kumsikia akiongea kwa muda mfupi, alibaini kuwa anaweza kuwa baba mzuri.

“Ni mtu ambaye ana sifa zote za kuweza kuwa mwanaume ambaye namtaka. Namchukulia kama kaka yangu yaani sijawahi kumfeel kimapenzi lakini nimekaa naye kwa muda mfupi, nimemuona ni mtu fulani mwenye busara. Ni mwanaume ambaye nikimuona nasema ‘this guy, I wish ningekuwa nina hisia za kimapenzi naye. Katika wasanii wote I wish my boyfriend angekuwa hivi,” Linah ameiambia 255 kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM.

Ameongeza kuwa Darassa anajua kuwa anakumbali na rapper huyo pia anamkubali Linah na ukaribu wao ni wa kama kaka na dada tu.

Msanii Rashid Abdallah Makwiro 'Chid Benz' ajiunga katika lebo ya WCB

Msanii maarufu wa miondoko ya kufoka/kurapu Rashid Abdallah Makwiro al maarufu kama CHID BENZ amejiunga rasmi katika lebo ya Wasafi Classic Baby WCB mchana Iliyo chini ya mwanamuziki machachari kabisa Diamond platnumz.

Taarifa hizi zimepatikana kupitia mtu wa karibu sana wa Babu Tale. Na pia kituo cha kuaminika cha redio yaani CloudsFM kimetaarifu mchana wa leo.....

Nisha na Wolper Wavutana, Kisa Viserengeti Boys vya Bongo Flava...

Mastaa wa bongo muvi, Salma Jabu ‘Nisha’ na Jacqueline  Wolper wamejikuta wakivutana mtandaoni baada ya Nisha kuandijka kitu ambacho Wolper alijibu na kusababisha Nisha kuibuka tena na kutoa ufafanuzi.

Nisha aliandika haya; kwenye hicha hii
“Mmoja kati ya hawa amejaa kwenye galary ya simu yangu na moyoni mwangu,otea A B C AU D? enhe. hivi sasa siweki hadharani maana nna phd ya kunyakuliwa.
sa hivi ni kumpost kwa mwendo kasiii yaani wengi wengi simtaji ng’ooo.
RAMADHAN QAREEM...sasa andika matusi ufungulie.
nimesubiri siku hii muda jmn dah watu wakiwa wamefungwa makufuli midomoni na mwezi(waislam/waikristo wote wanauheshimu”

Baada ya ujumbe huo wa Nisha ndipo Wolper alitoa maoni yake kwenye picha hiyo kwa kuandika hivi

Kisha Nisha Akajibu;


Ok guys kuna picture niliweka saa 4 asbh leo,za wasanii kadhaa wa music ambao niliweka na caption yangu kwa furaha zangu tu.
ila baada ya lisaa limoja ikaja coment hiyo ya msanii mwenzangu sikudhungumza chchte,i was like ok nikacheka tu.
then zikaja comments nyingi za kumuuliza kulikoni kuandika hivyo.
masaa mawili yaliyopita ukaandikwa waraka mzito mrefu unaosema. “Nisha aandaa show mtwara ya kumnasa Harmonize ila Wolper akagundua hilo akaamua kuongozana naye Harmo hadi huko kukwepa hilo (NA MANENO MENGI YA ZIADA YA UONGO.
ikimbukwe show imeshapita km week na haya maneno yamezuka leo baada ya hiyo coment.
guyz tuje kwenye point KWANZA KABISA SIJAMLENGA YYTE KWA NILIYEANDIKA NILIANDIKA KWA MAPENZI YNG KM NILIVYOANDIKA JANA STATUS YA VIDONDA VYA TUMBO,TENA HADI WADOGO ZNG NIKAWAAMBIA TAZAMA NACHEZA NA AKILI ZA WATU.
NIMESHANGAA HABARI ZA UONGO KUSAMBAZWA ZIDI YANGU TENA BAADA YA COMENT HII KWANGU.
POINT YA PILI KWA YYTE ANAYEULIZA NIMEANZA LINI UPROMOTA guyz mimi ni mfanyabiashara na kwenye pesa nipo,show ya MTWARA imenigharimu si chini ya ml.18 unadhani naweza poteza pesa zote hizo kisa mapenzi?sina ujinga huo wa akili.
NA SIJAWAHI KUMTAKA NA SITOTARAJI KWANZA SIJAZOEA KUPITA ANAPOPITA MTU HASWA NNAYEMJUA.
TATU nimeandaa show ingine ramadhan ya 13 DAR-ES-SALAAM inahusu ramadhan.
na nna SHOW SKUKUU YA IDD MOSS NA IDD PILI MIKOANI ZOTE MM NDO MUANDAAJI NA KUNA WASANII WAKUBWA TU JE HAO PIA NATAKA KUWANASA? HE.
IFIKE HATUA TUSIWE TUNABALANCE MTU MMOJA NA PIA SIO KILA ASIYEDHUNGUMZA NI MNYONGE SANA ILA KUNA WKT DRAMA HAZINA MUDA INABIDI UPIGE KAZI MAANA MAISHA YANAENDA MBELE HAYARUDI NYUMA.
NB:SHUKRAN KWA WEWE UNAYESAMBAZA UJUMBE HUU WA UONGO SINA CHA KUKWAMBIA NIMEPITIA MENGI MAKUBWA SO HILI KM NACHEZA MDAKO. (mwenye uelewa kaelewa chanzo cha story inayosambaa imetoka wapi,nimeandika hapa kwa manufaa ya mashabiki zangu wote watakaobahatika kusoma habari hizo za uongo.

Wasanii Wanaona ni Ufahari Kutoka Kimapenzi na Mastaa wa Kike Wenye Umri Mkubwa – Nay

Rapper Nay wa Mitego amesema wasanii wachanga wanajisikia ufahari kutoka kimapenzi na mastaa wa kike wenye umri mkubwa.
nay new2

Akizungumza katika kipindi cha Enewz cha East Africa Television Alhamisi hii, Nay wa Mitego amesema kuwa wasanii wachanga hawawezi kujizuia kutoka kimapenzi na mastaa wa kike waliyowazidi umri kwa kuwa walikuwa wanawatamani kwa muda mrefu.

“Mimi siwezi kuwalaumu hao vijana kuwa na uhusiano nao, unaju inaweza kuwa mtaani siku moja ulikuwa unawishi siku moja kuwa na mtu fulani, halafu ikitokea nafasi kama ile pale aah! Mtu hata upewe ushauri wa dizaini gani mtu ambaye ulikuwa ukimuona kwenye runinga anaingia katika kumi na nane zako mimi siwalaumu japokuwa wanatakiwa kuwa makini”, alisema Nay

Pia Nay alisema wasanii wengi wa kike, wamekuwa wakiutumia udhaifu huo ili kutembea na wasanii wachanga.

Picha: Muonekano Mpya wa Rapa Chidi Benz Baada ya Wiki Zaidi ya 20 Sober House

Hizi ni post mbili kutoka instagram za kituo cha Clouds Media kuhusu muonekano mpya wa msanii wa hiphop Tanzania Chid Benz.
Picha za post hizi ziliambatana na Ujumbe wenye maneno haya ” Muonekano mpya wa Chidi Benz Chuma…@CloudsTv pekee inakuonyesha safari za mwana harakati @Kalapina kwenye hatua za kusaidia vijana kuachana na janga la dawa za kulevya kwenye show ya #Harakati. #HarakatiNiVitendo “

Chidi Benz ni msanii aliyepata msaada mkubwa kutoka kwa meneja wa Diamond Platnumz mpaka kupelekea rapa huyu kukubali kwenda kupata matibabu baada ya kuwa mtumiaji wa dawa za kulevya wa muda mrefu jambo ambalo lilimrudisha nyuma kimuziki na maendeleo pia.
Share:

Baada ya FA Kupata Jiko… AY Naye Mbioni Kufunga Ndoa

KUFUATIA staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’ kufunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi, Helga wiki iliyopita, swahiba wake mkubwa, Ambwene Yessaya ‘AY’ amefunguka kuwa naye yuko njiani. Akizungumza na mtandao huu, AY anayebamba na Ngoma ya Zigo alisema kuwa ni jambo jema kwa rafiki na ndugu yake wa karibu (MwanaFA) kufunga ndoa hivyo imempa hamasa.

“Nimefurahi sana kwa swahiba wangu kufunga ndoa. Naamini FA amefungua ukurasa mpya katika maisha yake ya kuwa na mwenzake. Nami nipo njiani kumfuata Mungu akipenda,” alisema AY bila kumuweka wazi mwandani wake anayetarajia kufunga naye ndoa.
Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top