Loading...

Mimi ni mwanamuziki, Shilole ni mcheza shoo – Nuh Mziwanda

Msanii wa muziki, Nuh Mziwanda ameendelea kumponda aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kwa kudai sio mwanamuziki bali ni mcheza shoo.
nuhu

Muimbaji huyo wa wimbo ‘Jike Shupa’ amekuwa akitupiana maneno na Shilole kupitia mitandao ya kijamii toka wimbo huyo utoke.

Akiongea katika kipindi cha The Base kinachoruka katika runinga ya ITV, Nuh alisema hawezi shindana na Shilole kwa kuwa sio mwanamuziki.

“Mimi sitaki kiki, mimi mambo ya kiki nimeshayaacha, sasa hivi na fans base kwa ajili ya Jike Shupa,” alisema Nuh. “Ila yeye (Shilole) anajaribu kunichokonoa ili maisha yake yaende. Mimi ni mwanamuziki babu, siwezi kushindana naye, yule ni mcheza shoo,”

Shilole na Nuh hawakuachana vizuri, kila mmoja amekuwa akimtupia maneno machafu mwenzake.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top