Loading...

Magufuli ateua wakuu wa Wilaya 139, amtumbua Mulongo

John Magufuli, Rais wa TanzaniaRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt.Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.
Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.
Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali.
Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)
ARUSHA
Arusha – Mrisho Mashaka Gambo
Arumeru – Alexander Pastory Mnyeti
Ngorongoro – Rashid Mfaume Taka
Longido – Daniel Geofrey Chongolo
Monduli – Idd Hassan Kimanta
Karatu – Therezia Jonathan Mahongo
DAR ES SALAAM
Kinondoni – Ally Hapi
Ilala – Sophia Mjema
Temeke – Felix Jackson Lyaviva
Kigamboni – Hashim Shaibu Mgandilwa
Ubungo – Hamphrey Humphrey Polepole
DODOMA
Chamwino – Vumilia Justine Nyamoga
Dodoma – Christina Solomon Mndeme
Chemba – Simon Ezekiel Odunga
Kondoa – Sezeria Veneranda Makutta
Bahi – Elizabeth Simon
Mpwapwa – Jabir Mussa Shekimweli
Kongwa – John Ernest Palingo
GEITA
Bukombe – Josephat Maganga
Mbogwe – Matha John Mkupasi
Nyang’wale – Hamim Buzohera Gwiyama
Geita – Herman C. Kipufi
Chato – Shaaban Athuman Ntarambe
IRINGA
Mufindi – Jamhuri David William
Kilolo – Asia Juma Abdallah
Iringa – Richard Kasesela
KAGERA
Biharamulo – Saada Abraham Mallunde
Karagwe – Geofrey Muheluka Ayoub
Muleba – Richard Henry Ruyango
Kyerwa – Shaban Ilangu Lissu
Bukoba – Deodatus Lucas Kinawilo
Ngara – Kanali Michael M. Mtenjele
Missenyi – Kanali Denis F. Mwila
KATAVI
Mlele – Rachiel Stephano Kasanda
Mpanda – Lilian Charles Matinga
Tanganyika – Saleh Mbwana Mhando
KIGOMA
Kigoma – Samsoni Renard Anga
Kasulu – Martin Elia Mkisi
Kakonko – Hosea Malonda Ndagala
Uvinza – Mwanamvua Hoza Mlindoko
Buhigwe – Elisha Marco Gagisti
Kibondo – Luis Peter Bura
KILIMANJARO
Siha – Onesmo Buswelu
Moshi – Kippi Warioba
Mwanga – Aaron Yeseya Mmbago
Rombo – Fatma Hassan Toufiq
Hai – Gelasius Byakanwa
Same – Rosemary Senyamule Sitaki
LINDI
Nachingwea – Rukia Akhibu Muwango
Ruangwa – Joseph Joseph Mkirikiti
Liwale – Sarah Vicent Chiwamba
Lindi – Shaibu Issa Ndemanga
Kilwa – Christopher Emil Ngubiagai
MANYARA
Babati – Raymond H. Mushi
Mbulu – Chelestion Simba M. Mofungu
Hanang’ – Sara Msafiri Ally
Kiteto – Tumaini Benson Magessa
Simanjiro – Zephania Adriano Chaula
MARA
Rorya – Simon K. Chacha
Serengeti – Emile Yotham Ntakamulenga
Bunda – Lydia Simeon Bupilipili
Butiama – Anarose Nyamubi
Tarime – Glorious Benard Luoga
Musoma – Vicent Anney Naano
BEYA
Chunya – Rehema Manase Madusa
Kyela – Claudia Undalusyege Kitta
Mbeya – William Ntinika Paul
Rungwe – Chalya Julius Nyangidu
Mbarali – Reuben Ndiza Mfune
MOROGORO
Gairo – Siriel Shaid Mchembe
Kilombero – James Mugendi Ihunyo
Mvomero – Mohamed Mussa Utali
Morogoro – Regina Reginald Chonjo
Ulanga – Kassema Jacob Joseph
Kilosa – Adam Idd Mgoyi
Malinyi – Majula Mateko Kasika
MTWARA
Newala – Aziza Ally Mangosongo
Nanyumbu – Joakim Wangabo
Mtwara – Khatibu Malimi Kazungu
Masasi – Seleman Mzee Seleman
Tandahimba – Sebastian M. Walyuba
MWANZA
Ilemela – Leonald Moses Massale
Kwimba – Mtemi Msafiri Simeon
Sengerema – Emmanuel Enock Kipole
Nyamagana – Mary Tesha Onesmo
Magu – Hadija Rashid Nyembo
Ukerewe – Estomihn Fransis Chang’ah
Misungwi – Juma Sweda
NJOMBE
Njombe – Ruth Blasio Msafiri
Ludewa – Andrea Awesso Tsere
Wanging’ombe – Ally Mohamed Kassige
Makete – Veronica Kessy
PWANI
Bagamoyo – Majid Hemed Mwanga
Mkuranga – Filbert H. Sanga
Rufiji – Juma Abdallah Njwayo
Mafia – Shaibu Ahamed Nunduma
Kibaha – Asumpter Nsunju Mshama
Kisarawe – Happyness Seneda William
Kibiti – Gulamu Hussein Shaban Kifu
RUKWA
Sumbawanga – Khalfan Boniface Haule
Nkasi – Said Mohamed Mtanda
Kalambo – Julieth Nkembanyi Binyura
RUVUMA
Namtumbo – Luckness Adrian Amlima
Mbinga – Cosmas Nyano Nshenye
Nyasa – Isabera Octava Chilumba
Tunduru – Juma Homela
Songea – Polet Kamando Mgema
SHINYANGA
Kishapu – Nyambonga Daudi Taraba
Kahama – Fadhili Nkulu
Shinyanga – Josephine Rabby Matiro
SIMIYU
Busega – Tano Seif Mwera
Maswa – Sefu Abdallah Shekalaghe
Bariadi – Festo Sheimu Kiswaga
Meatu – Joseph Elieza Chilongani
Itilima – Benson Salehe Kilangi
SINGIDA
Mkalama – Jackson Jonas Masako
Manyoni – Mwembe Idephonce Geofrey
Singida – Elias Choro John Tarimo
Ikungi – Fikiri Avias Said
Iramba – Emmanuel Jumanne Luhahula
SONGWE
Songwe – Samwel Jeremiah
Ileje – Joseph Modest Mkude
Mbozi – Ally Masoud Maswanya
Momba – Juma Said Irando
TABORA
Nzega – Geofrey William Ngudula
Kaliua – Busalama Abel Yeji
Igunga – Mwaipopo John Gabriel
Sikonge – Peres Boniphace Magiri
Tabora – Queen Mwashinga Mlozi
Urambo – Angelina John Kwingwa
Uyui – Gabriel Simon Mnyele
TANGA
Tanga – Thobias Mwilapwa
Muheza – Mwanaisha Rajab Tumbo
Mkinga – Yona Lucas Maki
Pangani – Zainab Abdallah Issa
Handeni – Godwin Crydon Gondwe
Korogwe – Robert Gabriel
Kilindi – Sauda Salum Mtondoo
Lushoto – Januari Sigareti Lugangika.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top