Loading...

BREAKING NEWS: PEMBA KIMENUKA MABOMU YA MACHOZI YARINDIMA WATU ZAIDI YA 100 WAPIGWA MABOMU NA RISASI ZA MPIRA

Wakazi wa Pemba wamelalamikia Jeshi la Polisi kuvamia maeneo yao na kupiga mabomu ya machozi na kufanya doria usiku wa kuamikia juzi katika mitaa na vijiji mbalimbali kisiwani humo na kuzua hofu miongoni mwao.

Maeneo yaliyokabiliwa na hali hiyo ni pamoja na Mahuduthi, Kengeja, Mgagadu na Kiwani, Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba ambako polisi wanadaiwa kupiga mabomu ya machozi zaidi ya 100 na kutumia risasi za mpira kuwatawanya watu.

“Ilikuwa saa 1.30 usiku (wa kuamkia Jumamosi), gari za polisi zilifika kiamboni (kijijini) kwetu zikipiga misere kwa kasi, sote tukawa na hofu, watu walikimbia na kwenda kujificha, wengine waliumia na baadaye wakapiga mabomu mfululizo, sijui waliondoka saa ngapi maana tulijifungia ndani,” alisimulia Zuberi Said (34), mkazi wa Kiwani.

Baadhi ya wakazi wa vijiji hivyo walidai huenda hatua hiyo ya polisi ilitokana na matukio ya kuhujumu mali za viongozi wa Shehia yanayoendelea.

Inadaiwa kuwa watu wasiojulikana usiku wa kuamkia Ijumaa waliteketeza miti na mashamba yanayomilikiwa na Sabiha Mohamed Ali na Abdalla Makame Hamad, ambao ni mashekha wa Shehia za Kendwa na Kiwani wilayani humo.

Ilidaiwa watu hao pia waliteketeza migomba na mikarafuu mali ya viongozi hao na kusababisha hasara ya mamilioni ya fedha.

Mkuu wa Wilaya ya Mkoani, Hemed Suleiman Abdallah aliyefika kujionea uharibifu huo alisema: “Sijui sababu ni nini, ila huenda ni kutokana na siasa chafu zinazoendelea hapa.”

Alilitaka Jeshi la Polisi na askari alioongozana nao katika ziara hiyo kufanya uchunguzi haraka ili kuwabaini na kuwakamata watu waliohusika na vitendo hivyo. “Wala msisubiri baada ya miezi 20 ndipo mkaanza kuchukua hatua,” alisema.

Kamanda wa Polisi Wilaya ya Mkoani Pemba, Mohamed Salim aliyeambatana na Mkuu wa Wilaya Abdalla, alikiri kuwapo kwa hujuma na kuwatuma askari katika vijiji hivyo kufanya doria.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top