Loading...

Mazungumzo ya amani ya Burundi yaanza Arusha

Image copyrightREUTERS
Image captionMamia ya watu wameuwawa nchini Burundi, tangu Rais Pierre Nkurunziza kuamua kuania muhula wa tatu wa uongozi wa nchi.
Mazungumzo ya amani kuhusu Burundi yameanza mjini Arusha, Tanzania, baada ya kuahirishwa mara kadha.
Serikali ya Burundi, na baadhi ya viongozi wa upinzani wanahudhuria mazungumzo hayo, ambapo mpatanishi ni rais mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa.
Lakini kundi kuu la upinzani halikujumuishwa, kwa sababu serikali imesema, haitozungumza na watu, inaowaona kuwa wapiganaji.
Mamia ya watu wameuwawa nchini Burundi, tangu Rais Pierre Nkurunziza kuamua kuania muhula wa tatu wa uongozi wa nchi.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top