Loading...

KOCHA Jamhuri Kihwelo 'Julio' Ajigamba..Lazima Tuifunge Simba

 
Kocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo 'Julio' amesema atahakikisha anashinda mchezo huo ili Yanga iwe bingwa.

Mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya Simba dhidi ya Mwadui FC ni kesho Jumapili na inasubiriwa kwa hamu ile mbaya. Itapigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Yanga inaongoza ligi ikiwa na pointi 68 ikifuatiwa na Simba yenye pointi 58, wakati Azam ina pointi 57. Yanga na Azam zimebakiwa na michezo mitatu, huku Simba wakiwa nayo minne.

Simba ikishinda mechi zake zote ikiwemo hii na Mwadui, itafikisha pointi 70, hivyo Yanga na Azam zikipoteza mechi zake zilizobaki, Wekundu wa Msimbazi wanaweza kuwa mabingwa.

Julio ambaye amewahi kucheza na kufundisha Simba, alisema hataleta urafiki kwenye mchezo huo na amepanga kushinda ili Yanga ipate ubingwa rasmi.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top