Loading...

Clinton: Siwezi kushindwa na Bernie Sanders

ClintonImage copyrightGETTY
Image captionClinton anahitaji wajumbe 90 kupata ushindi
Mgombea urais anayeongoza katika chama cha Democratic nchini Marekani Hillary Clinton amesema haiwezekani iwe kwamba hatakuwa mgombea wa chama hicho katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Novemba.
Katika mahojiano na kituo cha runinga cha CNN, amesema anajivunia uongozi mkubwa mbele ya mpinzani wake wa pekee Bernie Sanders.
"Nitakuwa mgombea wa chama change,” ameambia CNN.
“Hilo limekamilika tayari, kimsingi. Haiwezekani hilo lisitokee.”
Bi Clinton ana idadi kubwa ya wajumbe, wajumbe 2,293 na anahitaji wajumbe 90 pekee kujihakikishia ushindi.
Seneta wa Vermont Bernie Sanders naye ana wajumbe 1,533 na anahitaji wajumbe 850 kushinda.
Lakini maafisa wa Sanders wanasema Bi Clinton hafai kudhani kwamba tayari ameshinda, wakitaja ushindi wa karibuni wa Bw Sanders katika majimbo ya Indiana, West Virginia na Oregon.
Image copyrightAP
Kwenye mahojiano hayo na CNN, Bi Clinton pia amemkosoa mgombea mtarajiwa wa chama cha Republican Donald Trump akisema hajahitimu kuwa rais wa Marekani.
Amesema mfanyabiashara huyo tajiri kutoka Marekani ni hatari kwa demokrasia Marekani na kwamba msimamo wake kuhusu sera ya kigeni ni hatari sana.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top