Loading...

Mahakama: Kubenea ana kesi ya kujibu.


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imesema Mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Saed Kubenea, ana kesi ya kujibu dhidi ya tuhuma za  kutoa lugha ya matusi kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.
 
Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi watatu wa upande wa Jamhuri.
 
Hakimu Simba alisema ushahidi uliotolewa unaonyesha maswali dhidi ya mshtakiwa na kwamba anatakiwa kupanda kizimbani kujitetea.
 
Alisema ushahidi wa upande wa utetezi utaanza kusikilizwa Machi 7, mwaka huu.
 
Wakili wa utetezi, Peter Kibatala, alisema upande wake unatarajia kuita mashahidi wanne akiwamo mshtakiwa.
 
Hakimu Simba alisema dhamana ya mshtakiwa inaendelea na kesi hiyo itaendelea kusikilizwa ushahidi wa utetezi Machi 7, mwaka huu.
 
Katika kesi ya msingi, Kubenea anadaiwa kuwa Desemba 14, mwaka jana, katika Kiwanda cha Tooku Garments kilichoko maeneo ya Mabibo External wilayani Kinondoni, Kubenea alitumia lugha ya matusi dhidi ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Makonda, hali ambayo ingesababisha uvunjifu wa amani.
CHANZO: NIPASHE

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top