Loading...

Sheria ya Facebook yaanza kuwabana watumiaji



Malisa Golisten
Sheria ya mtandao wa Facebook  imewafungia watu wanne wanaotumia mtandao huo  vibaya ikiwamo kukiuka sheria.

Mmoja wa waliopewa adhabu na mtandao wa Facebook, Malisa Golisten aliliambia gazeti hili kuwa amepewa adhabu ya kufungiwa kutumia mtandao huo kwa muda wa siku saba kutokana na kutolewa kwa taarifa na watu 50 kuwa anatumia mtandao huo kinyume na matakwa ya jamii yake

Pia amesema hivi karibuni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupitia kituo cha luninga cha TBC ilitoa elimu juu ya kutoa taarifa kwa umiliki wa mtandao.

Malisa amesema kulikuwa na ufahamu juu ya uwepo wa sheria hiyo ambayo mtandao wa Facebook ulikuwa unataka watu watoe taarifa juu ya uvunjifu wa sheria na maadili kama kutuma picha za ngono, kutoa taarifa ambayo siyo ya kweli na ya kichochezi.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top