Loading...

Pesa Tulizowekeza Kwenye Muziki zimeanza Kurudi- Navy Kenzo

Kundi la muziki, Navy Kenzo ambalo linaundwa na wasanii wawili, Nahreal pamoja na Aika, ni moja kati ya makundi machache ya muziki nchini ambayo yanawekeza pesa nyingi katika kuandaa kazi zao.
Navykenzo

Akizungumza na Bongo5 hivi karibuni, Nahreal amesema tayari wameshaanza kurudisha pesa zao ambazo wamekuwa wakiwekeza kwenye muziki kwa muda mrefu.

“Gharama ambazo tumetumia ni kubwa na tunajua muziki ni uwekezaji, lazima uwekeze, kwa hiyo mwanzo tulikuwa tunaweka pesa nyingi lakini hazikuwa zinarudi, so tumefika wakati pesa imeanza kuingia. Kama tour yetu imetupatia pesa fulani, pia wimbo wetu ‘Kamatia Chini’ umetupatia deal kubwa. Kwa hiyo pesa ambayo tuliwekeza inarudi kwa njia nyingi, makampuni, show, na issue nyingine,” alisema Nahreal.

Pia katika hatua nyingine Nahreal amewataka mashabiki wake kusubiria kazi mpya pamoja na kolabo za kimataifa.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top