Loading...

Bado Sijajua watu Wanaupendea nini Muziki wa Diamond Platnumz

Bongo ina wasanii wengi sana, kati yao 90% hawajui muziki kifupi ni wabovu akiwemo Diamond ila wanapendwa kupita maelezo, na 10% wanajua muziki kifupi ni wakali akiwemo Rama dee na Steve wa RnB ila cha kushangaza hawapendwi(muziki wao).

Sasa nashindwa kuelewa inakuwaje?? Mfano huyu Diamond miziki yake ni ya kawaida tu lakini raia wanamshobokea vibaya sana, kila ngoma anayotoa inakuwa ni national anthem lakini nikisikiliza mi naona ni miziki tu ya kawaida ambayo hata kwenye flash au laptop au memory card yangu siwezi kuweka.

Sijajua watu ni kwamba hawajui muziki au ni nini tatizo au ni ufreemason na uganga wa kupumbaza watu?? Kama ni mganga basi ni kiboko aisee, nasema ukweli ngoma za jamaa ninazozikubali ni Nitarejea na kesho, basi!

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top