Loading...

BREAKING NEWS>>> NI MUDA MFUPI TU BAAADA YA RAIS JOHN MAGUFU KUTEUWA MAKATIBU TAWALA 25 NA KUTUMBUWA WENGINE WANANE PAPO HAPO....

 

Rais John Magufuli 
Dar es Salaam. Rais John Magufuli amefanya uteuzi wa makatibu tawala wa mikoa 25 na kuwabwaga wanane, waliokuwa wanashikilia nafasi hizo.
Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi ilieleza kuwa kati ya makatibu tawala hao, 10 ni wapya wawili wamebadilishiwa vituo vya kazi na 13 wamebakishwa kwenye vituo vyao vya sasa.
Wapya ambao wataapishwa Ikulu kesho asubuhi ni Richard Kwitega (Arusha), Selestina Gesimba (Geita), Armatus Msole (Kagera) na Aisha Amour (Kilimanjaro).
Wengine ni Zuberi Samataba (Pwani), Albert Msovela (Shinyanga), Dk Angelina Lutambi (Singida). Jumanne Sagini anakwenda Simiyu, Dk Thea Ntara (Tabora) ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Zena Said (Tanga).
Makatibu tawala waliobadilishwa vituo ni Charles Pallangyo kutoka Geita kwenda Kigoma na Dk John Ndunguru kutoka Kigoma kwenda Morogoro.
Waliobakishwa vituo vya kazi ni Theresia Mbando (Dar es Salaam), Rehema Madenge (Dodoma), Wamoja Dickolagwa (Iringa) na Paul Chagonja (Katavi).
Wengine ni Ramadhan Kaswa (Lindi), Benedict Ole Kuyan (Mara), Eliakimu Maswi (Manyara), Mariam Amri (Mbeya), Alfred Luanda (Mtwara).
Kamishna Mathew Mtweve (Mwanza), Jackson Saitabau (Njombe), Symthies Pangisa (Rukwa) na Hassan Bendeyeko (Ruvuma).

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top