Loading...

Hatuwaogopi Wamisri, Kesho Tutawafunga - Samatta

Samatta amesema, Misri ni timu ngumu na anaamini watakuwa wamejiandaa vizuri kwasababu wanajua mechi ya kesho ndiyo itawapa tiketi ya kuelekea fainali za mataifa ya Afrika mwakani lakini ni lazima watafugwa kwani Stars itakuwa inachezea Uwanja wa nyumbani.

Samatta amesema, hawaangalii kama wananafasi ya kupita au hawana nafasi lakini muhimu ni kuweza kupata ushindi wa aina yoyote haijalishi ni zaidi ya goli tatu au chini ya goli tatu wanachoangalia wao kama timu ni ushindi na kuweza kuwapa raha watanzania.

Samatta amesema, wachezaji wenzake wote wapo vizuri na kila mchezaji mawazo yake ni kuweza kufanya vizuri hapo kesho na wanategemea ushindi na sio sare wala kufungwa kwani watapambana kama timu ya Taifa na sio mchezaji mmoja mmoja.

Samatta amewataka watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa ili kuipa sapoti timu yao na watahakikisha wanawapa watanzania furaha kwa kuweza kuibuka na ushindi katika mchezo huo.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top