Loading...

Nay wa Mitego Anaimba Hip Hop Kama Taarab, Abadilike – Gigy Money

Video vixen machachari, Gigy Money amedai ni muda wa rapper Nay wa Mitego kubadilika kwasababu anachokisikia kwenye nyimbo zake ni taarab na sio hip hop ya ukweli.

image

Gigy ambaye hapo awali amewahi kuzinguana na hitmaker huyo wa ‘Nasaka Pesa’ baada ya kutumika kwenye video ya Shika Adabu Yako ya rapper huyo na kutolipwa ujira wake, amemuambia mtangazaji wa Jembe FM ya Mwanza, JJ kuwa hip hop ya Nay imejaa uswahili mwingi.

“Inabidi abadilishe uimbaji wake uwe wa kisasa zaidi. Nay anaimba hip hop as taarab, imekuwa ni lugha ya mafumbo wakati hip hop ni zamani ilikuwa inatritiwa nyimbo sexy ambazo anasikiliza mtu akiwa ametulia,maneno unayasikia,” amesema Gigy. “Lakini yeye anataka kuimba vitu vingi katika muda mmoja halafu anaponda, so he is bad to me kwa asilimia 00.0.”

Kwa upande mwingine Gigy amesema msanii wa hip hop anayemkubali Tanzania ni Joh Makini.

“Anajielewa, hana skendo, yaani ana nyota yake kali, msafi,” amesisitiza.

“Anaimba vizuri, unamsikia hata kama ni M-Arusha, yaani R na L zinatofautiana.”

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright KAZI YANGU | Designed By AFROPIXELS MEDIA CO. LTD
Back To Top